ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, February 9, 2023

MELI KUBWA YA MV MWANZA HAPA KAZI TU KUSHUSHWA NDANI YA ZIWA VICTORIA KUENDELEA NA UKAMILISHWAJI WAKE

Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Huduma za Meli, Eric Hamissi amesema, Meli ya Mv Mwanza Hapa  ujenzi wake umefikia asilimia 82 hadi kukamilka kwake itakuwa imegharimu kiasi cha shilingi bilioni 109 na inatajiwa kushushwa ndani ya ziwa Victoria siku ya  February 12 mwaka huu kwa ajili ya kuendelea na hatua mbalimbali za ukamilishaji wake ili iweze kukamilika na kuweza kuanza kutoa huduma za usafirishaji katika nchi ya Kenya, Uganda, Sudani ya Kusini na hapa nchini.


Ushushwaji wa Meli ni zoezi nyeti sana tumepata msaada mkubwa kutoka kwa Jeshi la Wananchi la Tanzania,Kamandi ya Wanamaji, Polisi Marine,Jeshi la Zimamoto na baadhi ya wastafu ambao wako ktika taaluma hiyo ili kuhakikisha ili zoezi linafanyika kwa hali ya usalama kabisa nichukue nafasi hii kuwashukuru wadau wote serikali ya mkoa ikiongozwa na Mkuu wa Mkoa Adam Malima,Jeshi la Wananchi wa Tanzania pamoja na Jeshi la PolisI, Eric Hamissi - Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Huduma za Meli, MSCL.

Ujenzi wa Meli Duniani una hatua kubwa tatu, hatua ya kwanza ni kuweka msingi wa meli, hatua ya pili ndio hii tutaiona siku ya February 12, 2023, ya kushusha sasa meli kutoka kwenye chelezo kuweka kwenye maji na hatua ya tatu itafuata baadae baada ya miezi sita itakuwa ni kujaribu mitambo ya meli na kufanya safari za majaribio kabla ya kuanza safari rasmi, Eric Hamissi - Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Huduma za Meli Nchini, MCSL


Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Huduma za Meli Nchini, Eric Hamissi  katika tukio la ushushwaji wa meli mgeni rasmi anatarajia kuwa Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Makame Mbarawa, pamoja na wakuu wa mikoa yote inayozunguka kanda ya ziwa Victoria wakiwemo wakuu wa mikoa ya Kigoma na Tabora huku akiwaalika wakazi wote wa kanda hiyo kushuhudia tukio kubwa na la kihistoria la ushushwaji wa meli hiyo.

Meli ya Mv Mwanza Hapa kazi tu, ambayo ni kubwa kuliko zote katika ukanda wote wa maziwa makuu na itakuwa na uzito wa tani elfu tatu mia tano, itakuwa na urefu wa mita 92.6, pia itakuwa kuwa na kimo cha ghorofa 4 na upana wa mita 17, ina uwezo wa kubeba abiria elfu moja mia 2,mizigo tani 400 na magari kuanzia 20 kwa maana ya meli hiyo nchi yetu ya Tanzania inavunja rekodi ya kuwa na meli kubwa ambayo itaelea katika ziwa Victoria, Eric Hamissi, Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Huduma za Meli Nchini, MSCL.


Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.