ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Sunday, January 8, 2023

MWANAHARAKATI WA MAPENZI YA JINSIA MOJA KENYA AKIRI KUUA.


Mshukiwa wa mauaji Jactone Odhiambo amekiri kuwa alimtoa uhai aliyekuwa rafikiye Edwin Kiptoo maarufu kama Chiloba. actone Odhiamboamekiri kumtoa uhai Edwin Chiloba. Chanzo: Twitter 

Odhiambo amewaambia polisi hakuna haja ya kupoteza muda wakichunguza kifo hicho kwani yeye ndiye alitekeleza mauaji. 

Amesema sababu ya kuamua kumuua Chiloba ni machungu ya kusalitiwa kimapenzi kwani walikuwa na uhusiano wa mapanzi. 

Polisi wanasema mshukiwa huyo alisema alitekeleza mauaji hayo Januari mosi saa chache tu baada ya kuukaribisha mwaka moja wakiwa pamoja katika klabu moja maarufu mjini Eldoret. 

Makachero wanaochunguza kisa hicho wamesema kuna washukiwa wengine wawili ambao walisaida Otieno kutekeleza unyama huo. 

OCPD wa Langas alisema Odhiambo aliambia polisi kuwa ugomvi ulizuka kuhusu CHiloba kuwa na mpenzi mwingine. 

Wawili hao wamekuwa wakiishi kwenye chumba kimoja mjini Eldoret eneo la Chepkoelel ambapo majirani walisema hawakuwahi skia ugomvi. 

Aidha inaarifiwa kuwa hata baada ya Chiloba kuuawa, Odhiambo aliendelea kutumia simu yake na hivyo wengi hawakushuku kuna lolote limefanyika. 

Kwa wakati mmoja, majirani waliskia uvundo ukitoka nyumba ya awali hao na walipouliza, mshukiwa akawaambia kulikuwa na panya amefia ndani. 

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.