ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, January 5, 2023

KENYA: "KINOTI HAKUJIUZULU KUTOKA DCI NILIMFUTA KAZI" RAIS RUTO


Baada ya taarifa za Septemba 27, 2022 za Kujiuzulu kwa aliyekuwa Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI), George Kinoti, Rais #WilliamRuto amesema alimfuta kazi kutokana na kuongezeka kwa Mauaji na kutoweka kwa Raia kulikohusishwa na Polisi


Rais Ruto alielezea masikitiko yake kuhusu kupatikana kwa zaidi ya miili 200 ya Wakenya katika Mito na vichaka vya maeneo mbalimbali huku sababu za vifo zikiwa ni kitendawili, ambapo aliiagiza Mamlaka Huru ya Kusimamia Polisi (Ipoa) kuchunguza na kuwakamata waliohusika na mauaji hayo


Amesema, "Miili 30 huko #Yala, 17 #Garissa, kulikuwa na kontena hapa #Nairobi ambapo Watu walikuwa wakichinjwa katika Kituo cha Polisi, tulifikaje hapo? Ilikuwa ni Taasisi gani ya kihuni? Na ndio maana nilimfukuza huyo Kinoti, kwa sababu sio sawa"

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.