ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, December 22, 2022

KAMA MBAPE ANASEMA HIVI BILA SHAKA 'MESSI ANAHITAJI MAADUI WAPYA'


 Kylian Mbappe wakati akirejea mazoezini huku vyombo vya habari vikiwa na shahuku ya kutaka kujua atamtizama vipi aliyekuwa mpinzani wake kwenye Kombe la Dunia Leonel Messi:

"Tutakuwa na wasaa mzuri na Messi. Huu ni wakati mwingine bora zaidi. Nilifunga penati mbili na ya 3. Alifunga moja na ya 2.

"Alikuwa anafanya kazi zake Qatar na mimi nafanya yangu pia"

Katika ngazi ya Klabu tunafanana shauku zetu na matamanio, na tukifanya kazi pamoja yeye na Neymar... Tutafanya vivyo hivyo tena.....

Aliwahi kuniambia kazi yake ni kunisaidia ili nifanikiwe kama yeye, na kwa hilo ninamwamini.

Kwa huduma na msaada anaotoa kwangu na timu kwa ujumla....kamwe siwezi kumsema vibaya.

Na huwa analiongelea hili kwa kutuambia .. "Soka ni mchezo rahisi" .. Na ndiyo maana nami nafanya mambo kadhaa kuonekana rahisi.... siwezi kuukata mkono unaonilisha eti kisa vyombo vya habari, najifunza mengi kutoka kwa huyu mkongwe.

"Tulisawazisha ikawa 1-1 katika mchezo wa Kombe la Dunia, kisha 2-2, na baadaye 3-3 ,, lakini yeye yuko mbele kwa kila kitu,, kazi yangu ni kumsikiliza hata iweje....." alimaliza Mbape.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.