ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, December 1, 2022

AJALI YA ROLI LA MATOFALI YAUWA WATATU, YUMO DALALI MAARUFU WA JIJI LA MWANZA

NA ALBERT G. SENGO / MWANZA

WATU watatu wamefariki dunia kwa ajali iliyotokea mapema hii leo mkoani Mwanza maeneo ya Mataa Nyakato - sokoni. Tukio lililohusisha lori lililokuwa limebeba matofali kufeli breki katika mteremko wa kuelekea Nyakato National na hivyo kwenda kuyagonga magari yaliyokuwa yakisubiri ruhusa ya taa za kuongozea magari.


Magari matatu ya abiria (Hiace) na gari moja private yamehusika katika ajali hiyo. Dalali maarufu hapa Mwanza anaefahamika kwa jina la Mzee Shaaban Kumba ndiye mwenye gari private iliyogongwa ambaye amefariki papo hapo.


 Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Wilbroad Mutafungwa anashuka na taarifa zaidi kwa kina.








Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.