ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, November 24, 2022

MWANAMKE ASTUKIA MCHUMBA AMEKUWA AKICHEPUKA NA JIRANI SIKU MOJA BAADA YA KUJIFUNGUA.


Mwanamke mmoja amesimulia kwa mshtuko kugundua kuwa mpenzi wake, mwalimu wa kupiga mbizi, ni tapeli wa mapenzi. 

Claire Barnes Northcott aligundua kuwa mchumba wake amekuwa akimchiti na jirani yake siku moja baada ya kujifungua mtoto wao.

 Claire Barnes Northcott alifichua kwamba aligundua kuhusu tabia mbaya ya mchumba wake baada ya kujifungua mtoto wao. 

Kulingana na gazeti la The Sun, mama huyo wa mtoto mmoja alisema yeye na mpenzi wake, aliyetambulika kwa jina la Leury, walikuwa wachumba na walikuwa wamebakish miezi michache kabla ya harusi yao. Northcott alisema: 

 "Siku moja baada ya kujifungua mtoto wetu wa kwanza Mickayley, ndiyo siku ambayo niligundua kuwa mchumba wangu alikuwa na uhusiano wa kimapenzi wa zaidi ya miaka miwili." Alibaini kuwa uhusiano wao umekuwa hadithi ya mapenzi, na mchumba wake amekuwa akimuonesha mahaba matamu. 

"Leury alikuwa mtu wa mahaba sana hata sikujua kwamba alifanya chochote isipokuwa kunipenda. Nilidhani tulikuwa na uhusiano wa hadithi tamu. Nilipogundua kwamba alikuwa na uhusiano wa kimapenzi na jirani yake kwa miezi kadhaa niolishtuka sana," Northcott alisema.

 Northcott na mpenzi wake walikutana wakati wa harusi ya rafiki yake katika Jamhuri ya Dominika, ambako anafanya kazi kama mwalimu wa kupiga mbizi. 

Alieleza kwamba walioneshana mahaba, na walianza kuchumbiana, na mwaka mmoja baadaye, alimuomba awe mkewe na mama wa watoto wake. 

Alipojifungua, moyo wake ulivunjika vipande vipande baada ya jirani wa mpenzi wake kutuma picha zake akiwa na jamaa huyo. 

Mwanamke huyo alikiri kwamba alikuwa na uhusiano wa kimapenzi na Leury na alitaka kumwambia lakini alisubiri baada ya kujifungua kwake.

Alipomkabili Leury na taarifa hizo, alikiri bila kusita kuwa alikuwa akimhiti na kumfanya afutulie mbali harusi yao. "Alituchezea akili, familia yangu, na marafiki zangu," alisema. 

 iliripoti kwamba jamaa alifutilia mbali harusi yake baada ya kugundua mkewe alikuwa na watoto wawili na mwanamume mwingine. 

Katika video ya kusikitisha, alielezea uchungu wake alipofuta mipango ya harusi na kuvua viatu vyake vya harusi na suti. Licha ya juhudi kadhaa ya walioshuhudia kumtuliza, bwana harusi aliyekuwa amepandwa na mori alikataa kuendelea na harusi. 

Pia alidai kurejeshewa mahari aliyolipa. "Watoto 2? Nirudishie mahari yangu nachukua mahari yangu," alisema. 

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.