ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Tuesday, July 26, 2022

WAZIRI MCHENGERWA AONGOZA KIKAO CHA UJUMBE WA TANZANIA BIRMINGHAM UINGEREZA

 


Na John Mapepele

Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo. Mhe,  Mohammed Mchengerwa  ameongoza kikao cha maandalizi ya ujumbe wa Tanzania katika kikao cha Mawaziri wa Michezo wa Jumuiya ya Madola kitakachoanza leo Julai 26 mjini Birmingham, Uingereza. 


Kikao hicho ni maandakizi mahususi kabla ya uzinduzi rasmi wa mashindano ya michezo ya Jumuiya ya Madola ya mwaka huu yanayofanyika nchini Uingereza huku Tanzania ikiwa imeshiriki katika michezo hiyo.

Katika mashindano hayo kwa mara ya kwanza Serikali imetoa  motisha kubwa kwa wachezaji watakaofanya vizuri na kurejea na tuzo nchini.

Mhe. Mchengerwa amesema dhamira ya Serikali ni kuhakikisha   michezo inatumika kikakamilifu kuitangaza Tanzania kimataifa.

Aidha, amesema michezo ni ajira na uchumi mkubwa ambapo amesisitiza wachezaji wote kuwa wazalendo kujituma kufa na kupona kwa ajili ya taifa la Tanzania.

Amepongeza jitihada kubwa zinazofanywa na Serikali chini ya Rais Samia Suluhu Hassan za kuleta mapinduzi  makubwa kwenye sekta za michezo katika kipindi kifupi iliyopo madarakani.

Miongoni mwa motisha hizo amesema  Serikali itatoa kiasi cha  dola  10,000 za kimarekani kwa mchezaji atakayerejea na medali ya dhahabu, dola 7000 kwa medali ya Shaba na dola 5000 kwa medali ya fedha.

 Kikao hicho kimehudhuriwa na Balozi wa Tanzania nchini Uingereza, Mhe. Dkt, Asha-Rose Migiro, Mhe. Mussa Sima ambaye ni Mjumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Michezo Ndugu Saidi Yakubu pamoja na wajumbe kutoka Tanzania.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.