ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, May 21, 2022

SERIKALI IMETOA ZAIDI YA BILIONI 3 UKARABATI VYUO VYA SITA VYA WATOTO WENYE ULEMAVU -KATAMBI

 

Naibu Waziri toka Ofisi ya Waziri Mkuu, Patrobas Katambi akizungumza jambo Mwenyekiti  wa Watu Wenye ulemavu  toka Korogwe Vijijini Shaban Shekihiyo wakati wa ghafla ya ufunguzi wa chuo cha walemvu
Naibu Waziri toka Ofisi ya Waziri Mkuu, Patrobas Katambi akizungumza jambo Mwenyekiti  wa Watu Wenye ulemavu  toka Korogwe Vijijini Shaban Shekihiyo wakati wa ghafla ya ufunguzi wa chuo cha walemvu
Naibu Waziri toka Ofisi ya Waziri Mkuu, Patrobas Katambi kulia akicheza mziki na wanafunzi walemavu toka kituo cha YDCP kwenye ghafla ya ufunguzi wa Chuo cha walemavu


NA OSCAR ASSENGA,TANGA
 
SERIKALI ya awamu ya Sita inaoongozwa na Rais Samia Suluhu imetenga zaidi ya Shs bil 3 kwa ajili ya ukarabati wa vyuo Sita vya watoto wenye ulemavu nchini


Kauli hiyo imetolewa Jijini Tanga  na Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu kazi,vijana,ajira na wenye ulemavu Patrobas Katambi wakati wa ufunguzi wa Chuo cha Ufundi na marekebisho kwa watu wenye ulemavu

Katambi alisema Serikali inatambua umuhimu wa kundi hilo na ilitoa maelekezo ya kufanyiwa ukarabati wa vyuo hivyo ili kutoa fursa kwa jamii hiyo kupata elimu itakayowasaidia kujifunza ufundi utakao wanufaisha katika maisha yao.


Aidha aliitaja mikoa ambayo ina vyuo hivyo ni pamoja na Daresalaam,Tanga,Tabora,Mtwara,Singida na Mwanza ambapo alisema kuwa kama vyuo hivyo vitatumika vizuri idadi kubwa ya watoto walemavu inaweza kujitegemea na kuingia katika ajira kwa maslahi ya maisha yao na familia zinazowazunguka.
 
Katambi aliongeza kuwa Mh:Rais Samia Suluhu ameziagiza Wizara zote zihakikishe zinatoa ajira kwa asilimia 3 kwa kundi hilo la walemavu ili kuwaondolea dhana ya kuwa wategemezi na watu wasioweza kujiajiri ama kuajiriwa.


"Lazima haki ya elimu,afya na ajira zitekelezwe kwa mujibu wa sheria za Nchi yetu,unafikiri bila ya kuliwezesha kundi hili kielimu na ufundi,utawaajiri wapi,nazima tuwaandae na tunaweza kupata watumishi bora"Alisema Katambi.


Hata hivyo amemuagiza Katibu Tawala Mkoa kuhakikisha wanapata eneo kubwa kwa ajili ya ujenzi wa chuo hicho ambapo kitakuwa na uwezo wa kupokea wanafunzi walemavu toka Kanda nzima ya Kaskazini.


Kwa upande wa katibu Tawala Mkoa Tanga Pili Mnyema alisema wapo walemavu elfu tatu ambapo Mkoa inawatambua na Serikali imeweka mazingira rafiki ili kuweza kuwawezesha.


Mnyema alisema kwa mwaka huu wa fedha tayari  Halmashauri imetoa Shs Mil 121 ambayo ni asilimia 2 ya Shs Mil 600 kwa ajili ya kuwawezesha walemavu.
 
Nae Mkuu wa Chuo hicho Joharia Msuya alisema changamoto ya chuo ni pamoja na kuwa na walimu 3 wa kuajiriwa jambo ambalo linazorotesha ufanisi wa majukumu ya kila siku.


Msuya alisema mbali ya walimu na wafanyakazi wasiokuwa walimu pia eneo la chuo hicho ni dogo ungilinganisha na idadi ya wanafunzi inayotakiwq kuhudumiwa ambapo wanatoka mikoa 3.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.