ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, April 9, 2022

WILL SMITH APIGWA MARUFUKU KUSHIRIKI OSCAR KWA MIAKA 10.

 

Will Smith amepigwa marufuku kushiriki katika Oscars and matukio mengine ya Academy kwa miaka 10 baada ya kumchapa kibao muigizaji na mchekeshaji Chris Rock wakati wa hafla ya Oscars.


Academy of Motion Picture Arts and Science ambayo huandaa sherehe za kutoa tuzo, ilikuwa kwa njia ya mtanda Ijumaa kujadili hatua za kinidhamu. Smith aliomba msamaha kwa vitendo vyake na kujiuzulu kutoka Academy.


Smith alimchapa kibao Rock kwa kumfanyia utani mke wake ambaye alikuwa amekata nywele, ikiwa ni kutokana na hali ya kiafya ya ugonjwa unaojulikana kama alopecia ambao humfanya mtu kunyonyoka nywele.


Chini ya saa moja baadaye, alipewa tuzo ya muigizaji bora kwa uigizaji wakati kama “King Richard,” ambapo aliigiza kama baba wa nyota wawili wa tennis Venus na Serena Williams.


Katika taarifa yake, Academy ilisema kuwa Oscars “iligubikwa na tabia mbaya na isiyokubalika hata kidogo ambayo Bwana Smith aliionyesha jukwaani.”

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.