ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, April 9, 2022

WAAMUZI 6, KUCHEZESHA SIMBA Vs ORLANDO

 

Waamuzi watakaochezesha mchezo wa mkondo wa kwanza wa kombe la Shirikisho kati ya Simba SC dhidi ya Orlando Pirates ya Afrika Kusini wametangazwa na VAR itatumika katika mchezo huo utakaochezwa Aprili 17, 2022. Uwanja wa Benjamini Mkapa dar essalaam.


Katika mchezo huo itatumika teknolojia ya usaidizi kwa njia ya televisheni kwa waamuzi VAR. na kwa mujibu wa CAF michezo yote ya hatua ya robo fainali teknolojia hii itatumika. Lakini itakuwa ni kwa mara ya kwanza VAR inatumika nchini Tanzania.


Waamuzi watakaochezesha mchezo huo, Mwamuzi wa kati ni Haythem Guirat kutoka Tunisia, Mwamuzi msaidizi namba 1 (Line 1) ni Khalil Hassan wa Tunisia, msaidizi namba 2, (Line 2) ni Samuel Pwadutakam kutoka Nigeria na mwamuzi wa mezani yani Fourth official ni Sadom Selmi wa Morocco


Na waamuzi watakaosimamia VAR ni Ahmed Elghandour wa Misri na msaidizi ni Youssef Wahid.


Lakini pia katika mchezo huo klabu ya Simba imeruhusiwa kuingiza mashabiki Elfu 60 (60,000) uwanjani katika mchezo huu, ikiwa ni kwa mara ya kwanza msimu huu. Katika michezo iliyopita walikwa wakiruhusiwa kuingiza mashabiki Elfu 35 (35,000) ambao ulikuwa ni mpango wa kujinginga na maambukizi ya Uviko 19.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.