ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, March 10, 2022

WALIOSAMBAZA VIDEO ZA PROF JAY KUFUATILIWA.

 


Hospitali ya Taifa Muhimbili imelaani na kusema haijashiriki kusambaza video inayomuonesha Professor Jay akipambania uhai wake, katika chumba cha uangalizi maalum (ICU), na kusema hospitali inafuatilia ili kubaini chanzo cha video hiyo na kuchukua hatua stahiki.


Taarifa hiyo imetolewa na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano kwa Umma wa hospitali hiyo, Aminiel Aligaesha, na kusema kwamba imesikitishwa na kitendo hicho kwa kuwa ni cha kiwango cha juu cha ukosefu wa maadili.


Aidha, Aligaesha amewaomba wananchi na watumiaji wa hospitali hiyo kuendelea kuwa na imani nayo na kuendelea kuheshimu taratibu za hospitali.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.