ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, March 12, 2022

RAIS SAMIA AAGIZA ZIANDALIWE KANUNI ZITAKAZOONGOZA MIKUTANO YA SIASA.

 

raispicc

Rais Samia Suluhu Hassan akizungumza na Wajumbe wa Kikosi Kazi cha Kuratibu Maoni ya Wadau wa Demokrasia ya Vyama vingi vya Siasa leo tarehe 12 Machi, 2022, Ikulu Chamwino Mkoani Dodoma 

Rais Samia Suluhu Hassan ametoa agizo kwa Waziri wa Katiba na Sheria, George Simbachawene kuandaa kanuni zitakazoelekeza jinsi ya kufanya mikutano ya hadhara ya vyama vya siasa.

Taarifa iliyotolewa leo Jumamosi, Machi 12, 2022 na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, Zuhura Yunus imeeleza kuwa Rais Samia ametoa maelekezo hayo leo Jumamosi Machi 12, 2022 baada ya kupokea maazimio ya awali kutoka kikosi kazi alichokiteua cha kufuatilia hoja zilizojitokeza katika mkutano wa wadau wa demokrasia ya vyama vingi vya siasa uliofanyika Desemba 15-17, 2021 Dodoma.

Rais Samia amemwagiza Waziri huyo kushirikiana na Tanganyika Lawa Society (TLS) pamoja na Zanzibar Law Society (ZLS) kutengeneza kanuni hizo.

“Kikosi kazi hicho chenye wajumbe 24, na ambacho kinawajibika moja kwa moja kwa Mhe. Rais, kiliwasilisha maazimio hayo Ikulu Jijijni Dodoma. Maazimio hayo yamegawanyika katika makundi matatu ya muda wa utekelezaji” imeeleza taarifa hiyo.

Taarifa hiyo imeeleza kuwa azimio la muda mfupi ni uandaaji wa kanuni zitakazoelekeza jinsi ya kufanya mikutano ya hadhara ya vyama vya siasa.

“Baadhi ya maazimio ya muda wa kati ni pamoja na rushwa na maadili katika uchaguzi, ruzuku, elimu ya uraisa, huku masuala yanayohusu uchaguzi wa katiba mpya vikiwa ni mpango wa muda mrefu”

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.