ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, March 12, 2022

MASHINE YA KISASA YA UCHUNGUZI WA SARATANI ILIYOTENGENEZWA NA MWANAMKE YATUA BUGANDO MWANZA


Mtandao wa Maendeleo wa Aga Khan (AKDN) kwa kushirikiana na Shirika la Maendeleo la Ufaransa (AFD) umekabidhi Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Bugando mashine ya kisasa ya kufanya uchunguzi wa awali na matibabu ya saratani ya matiti yenye thamani ya Sh800 milioni. Mashine hiyo iliyo vumbuliwa na mwanamke na kutengenezwa na wanawake madaktri ni ya tatu katika nchi za Afrika Mashariki na ya pili nchini imenunuliwa na kutolewa chini ya mradi mtambuka wa saratani nchini (TCCP) unaotekelezwa kwa miaka minne tangu mwaka 2020. Akizungumza katika hafla ya kukabidhi mashine hiyo katika Hospitali ya Bugando, Meneja wa mradi wa TCCP, Dk Harrison Chuwa amesema mradi huo unalenga kuboresha vifaa tiba vya saratani, kuendeleza matibabu, kutoa elimu kwa watoa huduma ya afya na kufanya utafiti wa saratani nchini. Mkuu wa Idara ya Mionzi wa hospitali ya Aga Khan, Profesa Ahmed Jusabani amesema mashine hiyo ina uwezo wa kufanya uchunguzi wa saratani kwa watu 20 hadi 25 kwa siku.

Mkurugenzi wa huduma ya Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe Tamisemi, Dk Ntuli Kapologwe (wa tatu kulia) akisikiliza maelezo kuhusu mashine ya kufanya uchunguzi wa awali wa saratani ya matiti kutoka kwa mtaalam wa mionzi Bugando, Dk Margreth Magambo (hayupo pichani). Mashine hiyo imegharimu Sh800 milioni.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.