ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Sunday, March 13, 2022

MWANDISHI WA HABARI WA MAREKANI AUAWA UKRANE.

 


Mwandishi mmoja wa habari raia wa Marekani, Jumapili aliuawa kwa kupigwa risasi, na mwingine kujeruhiwa katika mji wa Irpin, kitongoji kilicho mstari wa mbele, wa mapigano, kaskazini magharibi mwa Kyiv, nchini Ukraine, madaktari na mashahidi wameliambia shirika la habari la AFP.


Mmarekani huyo ametajwa kama mpiga picha wa video wa miaka 50, Brent Renaud, wa New York.


Danylo Shapovalov, daktari wa upasuaji aliyejitolea kwa ajili ya ulinzi wa Ukraine, alisema mmoja wa Wamarekani alikufa papo hapo, na wa pili kupewa huduma ya matibabu.


Wanahabari wa AFP mjini Irpin, walisema waliuona mwili wa mwathiriwa. Mwathiriwa wa tatu, raia wa Ukraine, ambaye alikuwa kwenye gari moja na Wamarekani, pia alijeruhiwa.


Maafisa wa Ukraine walivilaumu vikosi vya Russia kwa shambulzi hilo, lakini hali halisi haikufahamika mara moja.


Wanahabari wa AFP waliripoti kusikia milio ya risasi mizinga katika eneo hilo.


Kadi ya utambulisho ya New York Times ilikuwa miongoni mwa karatasi alizokuwa nazo mfukoni mwanahabari huyo, na kusababisha kuenea kwa ripoti kwamba alikuwa mfanyakazi wa gazeti hilo.


Hata hivyo, naibu mhariri wa New York Times alisema kwamba Brent, alikuwa mpiga picha na mtengenezaji wa filamu mwenye kipawa ambaye alikuwa amechangia The New York Times kwa miaka ya nyuma.


Mashambulizi ya Russia dhidi ya Ukraine yameendelea kushabisha maafa, na kupelekea mailioni ya watu kukimbilia nchi kadhaa, majirani wa Ukraine.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.