ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Monday, March 7, 2022

MBUNGE ATOA BATI 10,CHAKULA KWA KAYA ZAIDI YA 200 ZILIZOEZULIWA NA UPEPO MKALI ULANGA

 

MBUNGE wa Jimbo la Ulanga Mkoani Morogoro Mh Salim Alaudin Hasham aliyevaa tisheti nyekundu katikati akiwa na wananchi walioathirika na nyumba zao kuezuliwa na upepo ambapo aliwatembelea na kutoa mabati 10 kwa kaya zaidi ya 200
MBUNGE wa Jimbo la Ulanga Mkoani Morogoro Mh Salim Alaudin Hasham aliyevaa tisheti nyekundu katikati akiteta jambo na wananchi walioathirika na nyumba zao kuezuliwa na upepo ambapo aliwatembelea na kutoa mabati 10 kwa kaya zaidi ya 200
MBUNGE wa Jimbo la Ulanga Mkoani Morogoro Mh Salim Alaudin Hasham aliyevaa tisheti nyekundu kulia akiwa na wananchi  walioathirika na nyumba zao kuezuliwa na upepo ambapo aliwatembelea na kutoa mabati 10 kwa kaya zaidi ya 200
MBUNGE wa Jimbo la Ulanga Mkoani Morogoro Mh Salim Alaudin Hasham aliyevaa tisheti nyekundu akikagua nyumba za wananchi  walioathirika na nyumba zao kuezuliwa na upepo ambapo aliwatembelea na kutoa mabati 10 kwa kaya zaidi ya 200
MBUNGE wa Jimbo la Ulanga Mkoani Morogoro Mh Salim Alaudin Hasham aliyevaa tisheti nyekundu akikagua nyumba za wananchi  walioathirika na nyumba zao kuezuliwa na upepo ambapo aliwatembelea na kutoa mabati 10 kwa kaya zaidi ya 200
MBUNGE wa Jimbo la Ulanga Mkoani Morogoro Mh Salim Alaudin Hasham aliyevaa tisheti nyekundu akikagua nyumba za wananchi  walioathirika na nyumba zao kuezuliwa na upepo ambapo aliwatembelea na kutoa mabati 10 kwa kaya zaidi ya 200


MBUNGE wa Jimbo la Ulanga Mkoani Morogoro Mh Salim Alaudin Hasham ametoa bati 10 kwa kaya zaidi ya 200  ambazo nyumba zao zimeezuliwa na upepo mkali jambo lililopelekea kukosa makazi.

Hatua hiyo inatajwa kwamba itawapunguzia ukali wa maisha wananchi ambao wamekumbana na hali hiyo kutokana na nyumba zao kuezuliwa na upepo mkali

Mbunge Salim Ameyasema hayo baada ya kukagua uharibifu huo uliotokea siku za hivi karibuni na kupelekea vijiji vya Gombe,Mwaya,Kichangani,Mbuga na Kivukoni kupata maafa hayo na baadhi ya wananchi kukosa makazi hadi sasa.

Jimbo hilo la Ulanga limekuwa likipata maafa hayo mara kwa mara kutokana na baadhi ya nyumba kukosa mapaa imara jambo linalopelekea upepo pamoja na mvua kuezua nyumba hizo kirahisi.

Mbunge pia ameahidi kutimiza ahadi  hiyo ndani ya wiki moja ili kila Mwananchi arejee kwenye makazi yake haraka na kuendelea na shughuli zao za maendeleo.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.