ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, March 26, 2022

JAMII IMESHAURIWA KUWEKA UTARATIBU WA KUPIMA MAGONJWA YA SARATANI KWANI YANATIBIKA.

 


Waandishi wa habari Mkoani Mwanza wamejengewa uelewa juu ya magonjwa ya saratani ili wakaielimishe jamii yenye uelewa mdogo  katika maradhi hayo.

 

Taasisi ya Aga Khan kupitia mradi wa mtambuka wa saratani (TCCP) umetoa mafunzo kwa waandishi wa habari 37 Mkoani Mwanza Machi 25,2022 katika ukumbi wa nyakahoja mradi huo unafadhiriwa na Shirika la Maendeleo la Ufarasa (AFD) kwa kushirikiana na  Taasisi ya Aga Khan (AKF) wenye thamani ya Euro13.3m.


 Akizungumza katika  mafunzo hayo Mwezeshaji, Brendalinny John amesema  lengo la mafunzo hayo ni kuwajengea uwezo waandishi wa habari juu ya kuelimisha jamii namna ya kujiepusha na maradhi ya saratani sanjari na kuripoti taarifa sahihi.


 Amesema ni wajibu wa kila mwandishi wa habari kuandika taarifa za ugonjwa wa saratani kwa usahihi na uhakika kwa kufuata maadili na kutoa elimu kwa jamii ili waweze kutambua suala hilo na kufuata matibabu kwani ugonjwa huo unatibika.


Kwa upande wake Dkt.bingwa wa magonjwa ya Saratani alieyebobea katika magonjwa ya mionzi Beda Likonda aliyekuwa mgeni rasmi katika mafunzo hayo kutoka hospital ya Kanda Bugando amesema kuwa kila mwaka Tanzania inapata wagonjwa wapya elfu 40000 wa magonjwa ya Saratani  ikiwa Saratani ya shingo ya kizazi ikiwa inaongoza.

 

Amesema kuna changamoto mbalimbali za kupambana nazo kama Nchi wakipata takwimu halisi ,kutoa elimu kwa jamii na wadau wa afya juu ya njia za kuepuka na kujilinda na ugonjwa huo na tiba shufaa inatakiwa izingatiwe ilikupambana na ugonjwa huo wa Saratani.


Dkt. Bingwa wa upasuaji kutoka hospitali ya rufaa ya mkoa ya Sekou toule, Athanas Ngambakubi mesema saratani ni ugonjwa unaosababishwa na kugawanyika kwa seli za kiungo chochote mwilini bila kufuata utaratibu wa kawaida.


Dkt. Ngambakubi amesema kuwa watoa huduma binafsi waweke bei rafiki kwa wagonjwa ili kuweza kuokoa maisha yao.


Ngambakubi ameishauri jamii kuweka utaratibu wa kuchunguza afya zao na kubaini mapema ugonjwa huo ambao unatibika.


 Amesema dalili za saratani kwa wanawake ni kutokwa damu ukeni, maji maji machafu yenye harufu kali, uvimbe, homa, kuathili mfumo wa hewa kupungua uzito, vidonda visivyo pona.


Naye Meneja ubia uwezeshaji na mawasiliano wa mradi wa mtambuka wa saratani,Sarah Maongezi amesema mradi huo wa miaka minne ambao unatekelezwa kwenye wilaya 13 za mkoa wa Mwanza na Dar es salaam kwa kushirikiana na timu za mkoa.


"Mradi huu utaboresha huduma za awali za saratani kwenye vituo 100 vya afya vya Mwanza 50 na Dar es saalam 50 japo kuwa upo katika mikoa miwili lakini manufaa yake yataenea nchi nzima"amesema Maongezi.


Amesema lengo la mradi huo ni kudumisha ushirikiano na tafiti kuhusu saratani, kuboresha miundo mbinu na vifaa tiba vya huduma ya saratani, kuendeleza na kukuza rasimali watu wa taaluma mbalimbali za matibabu ya saratani na uboreshaji wa huduma na uhamasishaji wa saratani katila jamii.


Amesema jamii inauelewa mdogo juu ya kutambua na kupima ugonjwa huo kwani ni vema wajitokeze kwa wingi kufanya matibabu mapema na kuweza kubaini tatizo.


Mradi huo ni wa miaka 4 unaotarajia kumalizika mwaka 2024 na unamatarajio ya kujenga hospitali ya Saratani yenye mashine mbili za kisasa za mionzi ya  nje na ya ndani ,gari la uchunguzi wa Saratani ambalo litakuwa na mashine ya uchunguzi wa awali wa Saratani ya matiti na kupata taarifa sahihi za Saratani ,viatarishi ikiwa ni pamoja na kupata huduma bora.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.