ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, December 17, 2021

MTOTO ALIYEZIKWA AONEKANA, KABURI LAKE LAFUKULIWA.

 


Mtoto Leonard Morisha (11), mkazi wa Kijiji cha Ngemo, Mbogwe mkoani Geita, aliyefariki dunia na kuzikwa Juni 27, 2017, anadaiwa kufufuka baada ya Oktoba 2020 kuonekana wilayani Kahama na wazazi wake wamempata Desemba 12, 2021 akiwa amekatwa mishipa ya ulimi na hawezi kuongea.


Kamanda wa Polisi mkoa wa Geita Henry Mwaibambe, amethibitisha kutokea tukio hilo baada ya kuomba kibali cha mahakama na kufanikiwa kufukua mahali alipokuwa amezikwa mtoto huyo na kukuta nguo ambazo amezikiwa zikiwa hazijachakaa pamoja na suruali ya aliyekuwa baba yake ambaye pia alifariki 2019.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.