ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, December 16, 2021

MMOJA AFARIKI KWA KUPIGWA NA RADI, 48 WAKOSA MAKAZI TANDAHIMBA.

 


Mtu mmoja amefariki baada ya kupigwa na radi huku wengine  48 wakikosa makazi katika kijiji cha Huruma kata ya Kwanyama wilayani Tandahimba baada ya mvua kubwa iliyoambatana na upepo mkali kunyesha na kuezua paa za nyumba zao.


Akizungumza baada ya kufika katika kijiji hicho mkuu wa Wilaya ya Tandahimba, Kanali Patrick Sawala amesema  mvua hiyo iliyoambatana na upepo mkali imeleta madhara makubwa katika kijiji hicho.


Ameeleza kuwa Serikali imejipanga kuimarisha ulinzi wa wanachi hao na mali zao katika kipindi hiki ambacho wameanza kurekebisha makazi yao.


"Hili eneo limekuwa lilikumbwa na athari za mvua na upepo mara kwa mara mnatakiwa kuimarisha nyumba zenu. Tunatoa pole kwa wafiwa na kaya zote 48 zilizokutwa na madhara haya tutaimarisha ulinzi ili kihakikisha kuwa mnakuwa salama nyie na familia zenu," amesema Sawala.

Diwani wa kata hiyo Hamza Barakali amesema  amepokea taarifa hizo kwa masikitiko  kutokana na mvua hiyo kuleta maafa kwa mwananchi wake.


"Mvua ilinyesha kubwa na iliambatana na upepo mkali na kusababisha mtu mmoja kufikwa na umauti, naungana na  wananchi wa kata yangu nitasimamia mazishi na kuungana na wananchi wote ambao eneo lao limeathirika."


"Kwaweli inasikitisha nimepita kwenye nyumba zilizofikwa na madhara kweli nimetokwa na machozi sio jambo rahisi vyakula, malazi makazi yote yanahitajika  ili wananchi hawa waweze kirudi katika hali zao za kawaida," amesema Barakali

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.