ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, December 17, 2021

DC MOYO: HAJARIDHISHWA NA KASI YA UJENZI WA MADARASA TARAFA YA IDODI,ISIMAN NA PAWAGA

 

Mkuu wa Wilaya ya Iringa Mohamed Hassan Moyo akiwa anakagua miradi ya majengo ya madarasa kwa ajili ya wanafunzi wanaotarajiwa kuingia kidato cha kwanza mwakani mwezi wa kwanza mwanzoni huku akiwa haridhishwi na kasi ya ujenzi wa madarasa ya fedha za UVIKO 19
Mkuu wa Wilaya ya Iringa Mohamed Hassan Moyo akiwa anakagua miradi ya majengo ya madarasa kwa ajili ya wanafunzi wanaotarajiwa kuingia kidato cha kwanza mwakani mwezi wa kwanza mwanzoni huku akiwa haridhishwi na kasi ya ujenzi wa madarasa ya fedha za UVIKO 19
Mkuu wa Wilaya ya Iringa Mohamed Hassan Moyo akiwa anakagua miradi ya majengo ya madarasa kwa ajili ya wanafunzi wanaotarajiwa kuingia kidato cha kwanza mwakani mwezi wa kwanza mwanzoni huku akiwa haridhishwi na kasi ya ujenzi wa madarasa ya fedha za UVIKO 19

 
 Na Fredy Mgunda,Iringa

Mkuu wa Wilaya ya Iringa Mohamed Hassan Moyo ameonesha kutoridhishwa na kasi ya ujenzi wa vyumba vya madarasa vinavyojengwa kupitia msaada wa fedha za Uviko 19 akionya kuchukua hatua dhidi wasimamizi wa ujenzi.

 

Akiwa katika ziara ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa vyumba hivyo katika Tarafa ya Idodi na Isimani alisema Serikali haiko tayari kushuhudia wanafunzi wakishindwa kuanza masomo kwa wakati kutokana na changamoto ya vyumba vya madarasa

 

Moyo aliwaagiza maafisa Tarafa pamoja na Watendaji wa kata ya vijiji yanapojengwa Madarasa hayo kuhakikisha vyumba vyote vinakamilika kwa wakati na kukabidhiwa kwa Serikali ifikapo Desemba 30 mwaka huu.

 

Mohamed Hassan Moyo Mkuu wa Wilaya ya Iringa amefika Tarafa ya Idodi na kujionea hali halisi ya maendeleo ya ujenzi wa vyumba vya madarasa vinavyojengwa kupitia fedha za mpango wa maendeleo kwa ustawi wa Taifa na mapambano ddidi ya Uviko-19

 

Alisema kuwa serikali imetoa kila kitu kwa ajili ya ujenzi wa madarasa ya wanafunzi wanatarajiwa kujiunga na kidato cha kwanza mwenzi wa kwanza mwaka 2022 hivyo madarasa yote ya wilaya ya Iringa yanatakiwa kukamilika kabla ya mwaka 2022 ili yatumike kwa wakati kama ilivyo kusudiwa na serikali.

 

Moyo alisema kuwa Serikali haiko tayari kuona madarasa hayo yakichelewa kukamilika na kuwaagiza wasimamizi wa ujenzi kuhakikisha yanakamilika kabla ya desemba 30.

 

Aliwahimiza maafisa watendaji kuwasilisha kwa mkurugenzi changamoto zilizo zinazowekza kukwamisha kasi ya ujenzi wa vyumba hivyo ili Ofisi ya Halmashauri iweze kuzipatia ufumbuzi wa haraka ili madarasa hayo yaweze kutumika kwa wakati kama ilivyokusudiwa

 

Katika hatua nyingine mkuu wa wilaya ya Iringa Mohamed Hassan Moyo alisema kwa zaidi ya asilimia themanini (80%) ya majengo ya madarasa yanayaojengwa katika Tarafa ya Idodi na Isimani yanaendelea vizuri licha ya changamoto ndogo ndogo ambazo zimejitokeza kwenye baadhi ya shule kwa usimamizi usiolizisha wa baadhi ya watendaji wake.

 

Katika Ziara hiyo ametembelea Tarafa ya Idodi katika Shule ya Sekondari Mlowa, Idodi, Makifu na shule shikizi ya Kitisi akiwaeleza kutorishwa na kasi ya ujenzi wakati katika tarafa ya Isimani alitembelea shule ya sekondari Furahia,Nyerere,Izazi,Isiman,Ilambilole na Kiwele na shule mbili shikizi katika Tarafa hiyo ambapo kwa kiasi kikubwa yamekamilika vikibakia vitu vidogo tu vya kumalizia.

 

Katika ziara hiyo ya kukagua ujenzi wa madarasa hayo wananchi wamekuwa wakimshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suhuru Hassan kwa kazi kubwa anayoifanya kwa kuleta maendeleo ya nchi na kuwapunguzia ugumu wa maisha wananchi wake.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.