ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, December 16, 2021

AWESO AMFUTA KAZI MKURUGENZI MAMLAKA YA MAJI MPANDA.

 


WAZIRI wa Maji Jumaa Aweso amemuondoa  katika Nafasi ya Kaimu Mkurugenzi wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Mpanda-Katavi Mikaya Gyimbi kwa kushindwa kutekeleza Majukumu yake kikamilifu na kwa weledi.


Aweso ametoa uamuzi huo baada ya kutembelea mradi wa ujenzi wa Tenki la maji na nyumba ya mlinzi iliopo halmashauri ya manispaa ya Mpanda mkoani Katavi na kubaini uzembe katika usimamizi wa mradi na thamani ya fedha iliyotumika.


Pia, Waziri Aweso ameagiza Mhandisi aliesaini mradi huu pamoja na mkandarasi aliyeutekeleza kufika mara moja kesho ofisi ya Mkuu wa Wilaya Mpanda mkoani Katavi kwa hatua zaidi.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.