ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Tuesday, November 30, 2021

TANZANIA IMEJIPANGA HIVI KUKABILIANA NA TISHIO LA WIMBI LA NNE LA UVIKO 19

 


Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Dkt Dorothy Gwajima amesema kuwa Tanzania ni miongoni mwa nchi mbalimbali Duniani zilizojiandaa kukabiliana na tishio la wimbi la nne  la UVIKO 19 ambapo hivi sasa pia katika baadhi ya nchi duniani imegundulika kuwepo kwa anuwai mpya ya kirusi kinachotambulika kwa jina la OMICRON.


Ametoa tamko la serikali dhidi ya mwenendo wa UVIKO 19 na Tishio la wimbi la nne la ugonjwa huo baada ya taarifa kuenea kutoka nchi mbalimbali Duniani ambazo zimeanza kuripoti ongezeko la visa vipya vya UVIKO 19 huku ikiripotiwa kuwepo kwa Tishio la kirusi kipya cha Omicron hali inayohitaji jamii kuchukia tahadhari zaidi.

Dkt Gwajima amesema kuwa takwimu zinaonyesha hadi kufikia tarehe 29 Novemba 2021 jumla ya waliothibitika kuwa na maambukizi Duniani watu 260,867,011 kati yao vifo 5,200,267 ambapo takwimu za zaTanzania zinaonyesha hadi kufikia 28 Novemba 2021 jumla ya watu waliothibitika kuwa na maambukizi ni 26,273 na vifo vilivyotoke ni 731 ambavyo vimetolewa taarifa.


Amesema kuwa jukumu la kinga dhidi ya magonjwa yote ni la kila mwananchi ambapo Serikali kupitia Wizara ya Afya na Wadau wake kwa pamoja wanasimamia utekelezaji wa afua mbalimbali ili kuwezesha jamii kujikinga na UVIKO 19 wakati serikali ikiwezesha upatikanaji wa chanjo hadi sasa dozi za chanjo 4,305,750 zimepatikana kwa ajili ya kuchanja wananchi 2,766,575 amesema Dkt Gwajima.


Aidha Dkt Gwajima amesema kuwa serikali imepokea chanjo ya Jansen dozi 1,227,400,Sinopharm dozi 2,578,400 na chanjo aina Pfizer hadi kufikia 28 Novemba 2021 jumla ya wananchi waliopata chanjo 1,520,275 sawa na asilimia 2.7 ya watanzania Wote.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.