ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Tuesday, November 30, 2021

UJERUMANI YAFIKIRIA KUCHUKUWA HATUA KALI KUKABILIANA NA WIMBI JIPYA LA CORONA.

 


Kansela wa Ujerumani anayemaliza muda wake, Angela Merkel, na mrithi wake, Olaf Scholz, wanatazamiwa hivi leo kufanya mkutano na mawaziri wakuu wa majimbo kujadiliana juu ya wimbi jipya la virusi vya corona, huku kukiwa na miito ya hatua kali zaidi kuchukuliwa dhidi ya aina mpya ya kirusi kinachosambaa kwa kasi ulimwenguni. 


Msemaji wa chama cha Walinzi wa Mazingira, Janosch Dahmen, ameliambia shirika la habari la dpa kwamba kuna haja ya kufungwa baadhi ya shughuli za kawaida kwenye majimbo mengi ya nchi. 


Waziri mkuu wa jimbo la Bavaria kutokea chama cha CSU, Markus Soeder, ametowa wito wa ushirikiano na hatua kali zaidi. 


Hayo yanakuja wakati Mahakama Kuu ya Kikatiba ikiwa leo imetoa hukumu yake ya kwanza ambapo imesema kuweka zuio la shughuli za maisha na uhuru wa watu katika kuzuwia kusambaa kwa virusi vya corona kulikuwa halali.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.