ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Tuesday, November 30, 2021

AMCHOMA MTOTO SEHEMU ZA SIRI NA MOTO WA SIGARA.

 


Jeshi la Polisi mkoani hapa,linamshikilia Apolikarp Mushi kwa tuhuma za kumuunguza sehemu za siri kwa moto wa sigara, mjukuu wake wa kiume pamoja na kumtegua nyonga kwa kutumia kitu kizito.


Mushi anayeishi kijiji cha Uru Kyaseni wilayani Moshi mkoani Kilimanjaro, anadaiwa kumfanyia vitendo hivyo mtoto huyo mwenye umri wa mwaka mmoja na miezi sita anayeishi naye baada ya kutelekezwa na mama yake mzazi.


Anadaiwa kumfanyia ukatili huo kwa muda mrefu sasa ikiwemo vipigo vilivyopelekea mifupa ya nyonga kutenguka na kuchomwa na sigara sehemu za uume wake na kumsababishiavidonda.


Jana, Mwananchi lilishuhudia sehemu za mwili wa mtoto huyo ikiwamo miguuni, mapajani, makalioni na usoni zikiwa na majeraha huku akionekana kuwa na maumivu makali.


Katika mwili wa mtoto huyo kuna majeraha mengine ya mouda mrefu.


Akizungumzia tukio hilo Kamanda wa Polisi mkoani hapa,Simon Maigwa alithibitisha kutokea kwa unyama huo.


Maigwa alisema wanamshikiliza babu wa mtoto huyo na wameshaandaa jalada kwa ajili ya kulipeleka kwa Mwanasheria wa Serikali kwa hatua zaidi.


“Tunalifahamu tukio hilo, hatua zaidi zinaendelea, mtuhumiwa yupo mahabusu kwa ajili ya taratibu za kisheria,”alisema Maigwa.


Akizungumzia hali ya Mtoto huyo,baada ya kufikishwa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Mawenzi, Dk Tumaini Mtui, “Mtoto alipofikishwa hapa alikuwa hawezi kutembea na alikuwa amevimba sana mwili , tulimfanyia vipimo tulibaini alivunjika nyonga za upande wa kulia na kushoto na zilikuwa na mpasuko unaonekana umetokana na kipigo.Tumempa dawa, anatakiwa kupumzika ndani ya mwezi mmoja na kuhudhuria klinki ya mifupa”alisema Dk Mtui.


Kwa upande wa bibi mlezi wa mtoto huyo,Maria Masao alisema “Mara nyingi nimekuwa nikitoka asubuhi kwenda kwenye shughuli zangu na kurudi jioni,sasa juzi niliporudi nikamkuta yupo vibaya, yaani amevimba na mwili wake una majeraha kila mahali,ilinibidi niombe msaada kwa majirani ambapo nilipata msaada wa polisi,”alisema Masao na kuongeza.


“Nikimuuliza ananitishia kunipiga na panga na anasema atampiga hadi amuue, yaani hata hapa nyumbani hakuna jirani anayethubutu kuja kutokana na ukorofi wa huyu baba,”alisema mama huyo.


Mmoja wa majirani wa mtoto huyo,Gaudence Njau alisema , “Kwa kweli huyu mtoto ananyanyasika sana na amefanyiwa ukatili wa kila namna baada ya kuona unazidi ilibidi sisi wenyewetuingilie kati maana mtoto bado ni mdogo na anachofanyiwa hakiendani naye,”alisema jirani huyo.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.