ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, November 17, 2021

NGOMA ZA USIKU ZAPIGWA MARUFUKU TANDAHIMBA.

 


Mkuu wa Wilaya ya Tandahimba, Kanali Patrick Sawala amepiga marufuku ngoma za usiku zinazochezwa katika wilaya hiyo akisema zimekuwa chanzo cha watoto wa kike kupata mimba na kushindwa kutimiza ndoto zao.

Akizungumza na wananchi alipotembelea Kata ya Mihambwe amesema kuwa wakati wa kuchezwa ngoma hizo watoto wengi wa kike wamekuwa wakipata ujauzito wakiwa na umri mdogo.

Amesema kuwa hali hiyo imemsukuma kupiga marufuku ili kuwasaidia watoto wakike waweze kusoma na kutimiza malengo yao bila kuwa na vizuizi vya ujauzito.

“Wakati wa kuchezwachezwa hizi ngoma mimba ndio zinakuwa nyingi kwa watoto shuleni mbali na wanaopata ujauzito shuleni hii inamdidimiza mtoto wa kike anashindwa kusoma anashindwa kufikia malengo yake na kukatisha ndoto zake”

“Kwa jambo hili hatutafumbia macho mimi sizuii mila na desturi kufanyika hapana na sijaja hapa kuzuia lakini twendeni na utaratibu sisi ni mashahidi mimba nyingi zinapatikana usiku” amesema Kanali Sawala na kuongeza

“Ndio maana nimeamua kuwa ngoma za usiku nimezuia kwa sasa msihangaike kuomba vibali mila zingine ziendelee kufanyika lakini sio ngoma za usiku”

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.