ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, November 24, 2021

MALIKAH SHABBAZ: MWANA WA KIKE WA MALCOM X AFARIKI.

 


Malikah Shabazz, mwana wa mwanaharakati wa haki za kibinadamu aliyeuawa Malcom Xalipatikana amefariki siku ya Jumatatu nyumbani kwake Brooklyn, mjini New York, kwa mujibu wa polisi.

Shabbaz mwenye urmi wa miaka 56 , alikuwa kitinda mimba wa wasichana sita wa mwanaharakati huyo maarufuambaye miaka 1960 alipigania kuwezeshwa kwa Wamarekani weusi.

Shabbaz alipatikana akiwa amepoteza fahamumwendo wa 4.40 jioni Alitangazwa kufariki muda mfupi baadaye.

Habari hizo zinajiri siku chache tu baada ya wanaume wawili waliopatikana na hatia ya kumuua Malcolm X, Muhammad Aziz na Khalili Islam kuondolewa makosayamuaji yake na mahakama ya mjini New York.

Mapema mwaka huu , Watoto wa kike wa shujaa huyo waliomba kwamba uchunguzi ufunguliwe upya , wakidai kwamba kuna Ushahidi mpya.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.