ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Tuesday, August 10, 2021

UTEUZI WA WANASHERIA WA KUSIKILIZA KESI YA DHULUMA ZA KINGONO DHIDI YA MSANII R.KELLY WAANZA.

 

Msanii wa R&B R. Kelly amefika mahakamani mjini New York,huku uteuzi wa wanasheria katika kesi ya dhulma za kingono dhidi yake ukianza.

Inajiri zaidi ya miaka miwili baada ya msanii huyo kushtakiwa kwa unyanyasaji wa wanawake na wasichana wadogo kwa karibu miongo miwili.

Mwimbaji huyo aliyeshinda Tuzo ya Grammy anakabiliwa na mashtaka ya unyanasaji wa kingono dhidi ya watoto, ujambazi na rushwa. Amekanusha mashtaka

Wanasheria wanaotarajiwa kuongoza kesi hiyo wanahojiwa ikiwa wanaweza kuwa na mawazo huru katika kesi hiyo.

Baada ya majaji kuteuliwa, kesi inatarajiwa kuanza Agost18 na huenda ikaendelea kwa wiki kadhaa.Msanii huyo mwenye umri wa miaka 54 akipatikana na hatia huenda akafungwa jela kwa miongo kadhaa.

Kesi dhidi yake pia imewasilishwa katika mahakama ya Illinois na Minnesota.

Alipoulizwa jinsi anavyojihisi,wakili wa Kelly,Deveraux Cannick aliliambia shirika la Habari la AFP: "Ni sawa na Jumatatu nyingine."

Kelly, mmoja wa wasanii nyota wa miondoko ya R&B miaka ya1990, amekuwa akizuiliwa tangu Julai mwaka 2019.

Kesi ya New Yorki inamtuhumu mwimbaji huyo–ambaye jina lake halisi ni Robert Kelly –kwa kuongoza kundi la mameneja , walinzi wa kibinafsi na wengine ambao waliwaanda wanawake na wasichana kwa ajili ya kufanya ngono.

Waendesha mashtaka wanasema wahasiriwa waliteuliwa katika matamasha na maeneo mengine.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.