ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, August 12, 2021

RAIS WA MADAGASCAR ALIVUNJA BARAZA LA MAWAZIRI

 

 Rais wa Madagascar Andry Rajoelina amelivunjilia mbali baraza lake la mawaziri.

Ofisi yake haikutoa sababu, lakini Jumapili Bw Rajoelina alisema kutakuwa na hali ya kushindwa ndani ya serikali - "kama katika timu ya mpira wa miguu" - mabadiliko yangehitajika.

Kufutwa kwa baraza hilo kumekuja baada ya ripoti za njama iliyofeli ya kumuua rais ambaye ni kiongozi wa zamani wa mapinduzi huko Madagascar.

Zaidi ya washukiwa 20 - wakiwemo 12 kutoka kwenye jeshi - wamekamatwa. Bwana Rajoelina alikua rais wa kisiwa hicho miaka miwili iliyopita - baada ya mzozo wa kisheria uliogubika uchaguzi huo.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.