ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, August 12, 2021

PETER BANDA APEWA JEZI YA MIQUISSONE

 


Mchezaji mpya wa klabu ya Simba Peter Banda amekabidhiwa jezi namba 11 ambayo hapo awali ilikuwa ikitumiwa na Luis Miquissone ambaye anahusishwa kujiunga na miamba ya soka barani Afrika klabu ya Al Ahly ya huko Misri. 

Banda alijiunga na wekundu wa Msimbazi mwezi Agosti 3 mwaka huu akitokea Nyasa Big Bullets ya nchini Malawi kwa mkataba wa miaka mitatu.

 Mabingwa hao wa Tanzania hivi sasa wapo nchini Morocco ambako wameweka kambi yao kwa ajili ya maandalizi ya msimu mpya ujao.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.