ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Monday, February 24, 2020

KABENDERA AKUTWA NA HATIA, AHUKUMIWA KULIPA FIDIA NA FAINI MILIONI 273


Mahakama ya Kisutu imemuhukumu Mwanahabari Erick Kabendera kulipa fidia na faini ya Sh. Mil 273 baada ya kukiri makosa ya utakatishaji fedha na kukwepa kodi, tayari ameshaingiza Tsh. Mil 100 kwenye akaunti ya Serikali na ameachiwa huru huku akitakiwa kulipa fedha iliyobaki ndani ya miezi sita.

Hukumu hiyo imetolewa na Hakimu Mkazi Mkuu Janeth Mtega baada ya Kabendera kusota rumande kwa takribani miezi sita.

Katika kesi hiyo Kabendera anakabiliwa na kesi ya uhujumu uchumi yenye mashtaka matatu likiwemo la utakatishaji wa TSh.Mil 173.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.