ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, January 29, 2020

UJIO WA MV ILEMELA SASA WAMPA USINGIZI MBUNGE ANGELINA MABULA.


Ni dhahiri kuwa changamoto ya usafiri kwa wananchi wa eneo kati ya Kayenze na kisiwa cha Bezi wilayani Ilemela mkoani Mwanza sasa inakwenda kuwa historia mara baada ya kuanza majaribio ya usafiri na usafirishaji jumanne ya tarehe 28 Januari 2020.

Akizungumza mbele ya mamia ya wananchi Mbunge wa Jimbo la Ilemela Dkt. Angeline Mabula amekiri kuwa "Kweli ukitaka maendeleo wahitaji kuwa na ndoto kubwa" kwani wakati wa ahadi za uchaguzi 2015 moyo ulimsukuma kutamka ndoto yake hiyo kwa wakazi jimboni mwake lakini ilimnyima usingizi akiwaza na kuwazua nini kitatokea iwapo ahadi hiyo isinge kamilika.

Mabula amemwaga sifa nyingi kwa Rais wa Serikali ya awamu ya Tano ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akidai kuwa ndiye aliyempa kiburi na kujiamini kupitia historia ya utendaji wake.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.