ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Tuesday, January 14, 2020

JAMBO FOOD PRODUCT CO LTD WAINGIZA BIDHAA 3 SOKONI KWA MPIGO


Jambo Apple Crush Soda, Jambo Ubuyu na Jambo Ukwaju ni bidhaa tatu zilizoingizwa sokoni hivi karibuni na Kiwanda cha kutengeneza vinywaji baridi cha Jambo Food Products chanya maskani yake mjini Shinyanga nchini Tanzania. Hamis Salum ni mmoja kati ya Wakurugenzi waandamizi wa kiwanda hicho akiwa ameambatana na Meneja wa Masoko wa Kampuni hiyo hapa wanakupa taarifa zaidi. KUHUSU KIWANDA Kiwanda cha Jambo Food Products Company Limited kinachojihusisha na uzalishaji wa vinywaji baridi ikiwemo soda, juisi na maji kimejichukulia umaarufu wa bidhaa zake bora ambazo zinapendwa na watu wa rika zote kutokana na uhalisia wake. Kiwanda hicho ambacho kilizinduliwa na Rais Dkt. John Pombe Magufuli, mnamo Januari 13, mwaka 2017, hadi sasa kimekuwa moja wa viwanda vya uzalishaji bidhaa bora za viwango vya kimataifa toka hapa nchini, vywenye radha murua kukufanya ujisikie fresh kabisa muda wote, kuupa mwili nguvu na mzuka zaidi, afya bora na kukuburudisha. Jambo wanazalisha na kusambaza vinywaji aina mbalimbali kwa jumla na rejareja. Vinywaji kama, Jambo Malta Lemon, Jambo Apple, Jambo Embe, Jambo Energy, Jambo Malta Pineapple, Jambo Lemon, Jambo Vito, Jambo Orange, Jambo Drinking Water na nyingine kibaooooo! Kiwanda cha Jambo kipo Shinyanga Mjini. Simu: +255622666692 au +255622666680 Email: info@jambogrouptz.net. Website: https://jambogroup.co.tz

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.