ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Monday, December 23, 2019

KAMISHNA WA OPERESHENI NA MAFUNZO YA JESHI LA POLISI, CP LIBERATUS SABAS, AMEFUNGA MAFUNZO YA ASKARI WA KIKOSI MAALUM CHA ULINZI MPAKA WA TANZANIA NA MSUMBIJI PAMOJA NA ULINZI WA AMANI KIMATAIFA KILELEPORI NA WEST KILIMANJARO.


 Kamishna wa Operesheni na Mafunzo ya Jeshi la Polisi, CP Liberatus Sabas akisalimiana na wakufunzi wa askari wa Kikosi Maalum kitakachosimamia Ulinzi wa Amani katika Mpaka wa Tanzania na Msumbiji huko mkoani Mtwara katika Mto Ruvuma ambapo kumekuwa kukitokea mauaji ya mara kwa mara kwa raia wema yaliosababishwa na wahalifu kutoka Nchini jirani ya Msumbiji. (Picha na Jeshi la Polisi)
 Kamishna wa Operesheni na Mafunzo ya Jeshi la Polisi, CP Liberatus Sabas akiongea na askari  wanaohitimu mafunzo ya usimamizi wa Ulinzi katika Mpaka wa Tanzania na Msumbiji yaliofanyika katika pori la West Kilimanjaro mkoani Kilimanjaro.(Picha na Jeshi la Polisi)
 Kamishna wa Operesheni na Mafunzo ya Jeshi la Polisi, CP Liberatus Sabas akimkabidhi cheti cha ukufunzi bora Kamishna Msaidizi wa Polisi ACP William Mwampagale wakati akifunga mafunzo ya askari wa Ulinzi wa Amani Kimataifa Kilelepori mkoani Kilimanjaro.(Picha na Jeshi la Polisi)
 Kamishna wa Operesheni na Mafunzo ya Jeshi la Polisi, CP Liberatus Sabas wa tatu kutoka kushoto kwa waliokaa akiwa katika picha ya pamoja Maafisa wa Jeshi la Polisi, wakufunzi wa ndani pamoja na wakufunzi wa umoja wa kimataifa baada ya kufunga mafunzo Kilelepori mkoani kilimanjaro. (Picha na Jeshi la Polisi)
Kamishna wa Operesheni na Mafunzo ya Jeshi la polisi, CP Liberatus Sabas akisalimiana na wakufunzi wa Askari wa Kikosi Maalum kinachotarajiwa kujiunga na vikosi vingine vya Ulinzi wa Amani Kimataifa kwaajili ya kusimamia amani katika nchi au mataifa yenye migogoro. (Picha na Jeshi la Polisi)

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.