ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Sunday, December 1, 2019

ARSENAL YAKALIWA KOONI NA NORWICH EPL, AUBAMEYANG ADUNGUA MBILI.


Klabu ya soka ya Arsenal imetoka sare na katika mchezo wao wa kwanza dhidi ya Norwich City katika mchezo wa ligi kuu Uingereza wakiwa na kocha wao mpya wa muda Freddie Ljungberg.

Katika mchezo huo ambao Arsenal walikuwa ugenini wametoka sare ya kufungana mabao 2-2.

Norwich ndio walikuwa wa kwanza kupata bao dakika ya 21 kupitia kwa Teemu Pukki lakini Arsenal walisawazisha dakika ya 29 kwa njia ya penalti kupitia kwa Pierre-Emerick Aubameyang.

Hata hivyo Norwich walipata bao dakika mbili za nyoogeza kipindi cha kwanza kupitia kwa Todd Cantwell, lakini Aubameyang alisawazisha tena dakika ya 57.

Kwa matokeo hayo sasa Arsenal inashika nafasi ya nane ikiwa na alama 19 wakati Liverpool ikiongoza ligi hiyo ikiwa na alama 40.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.