ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, August 1, 2019

iMES, Imekuja kwa wakati Muafaka

 Mataalam kutoka OR-TAMISEMI, Fatma Yusuph, akitoa msaada wa kiutaalam kwa wataalam wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela, wakati wa zoezi la uingizaji wa taarifa katika mfumo wa iMES.
 Mtaalam wa TEHAMA, kutoka Mradi wa Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma nchini, Milton Ndosi, akitoa ufafanuzi wa jambo wakati wa zoezi la uwandani kwenye Jiji la Mwanza.
 Limi George, Afisa Ugavi Manispaa ya Ilemela, akiwa anaingiza takwimu katika mfumo wa iMES wakati wa zoezi la uwandani katika Manispaa hiyo. (Picha zota na Atley Kuni-TAMISEMI)
Afisa Takwimu kutoka OR-TAMISEMI, akitoa maelezo ya awali juu ya Mfumo wa iMES, kwa wataalam wa Jiji la Mwanza.

iMES, Imekuja kwa wakati Muafaka
Na. Atley Kuni- Mwanza
Wataalam kutoka Idara na Vitengo wa Manispaa ya Ilemela mkoani Mwanza, wamesema Mfumo jumuishi wa Ufatiliaji na Tathimini (integrated Monitoring and Evaluation System-iMES), umekuja kwa wakati na enzi muafaka, wakati huu ambao matumizi ya takwimu ni hitaji la kila nyanja katika kusukuma gurudumu la maendeleo.
Wakiwa katika zoezi la pamoja za uingizaji wa takwimu katika mfumo, wataalam hao wamesema, ile hali yakukimbizana na taarifa pindi zinapo hitajika sasa litakuwa mwanzo na mwisho wake.
Limi George, Afisa Manunuzi katika Manispaa hiyo anasema kwamba, kwakuwa mfumo ni web base, haita malazimu mtaalam kuanza kutembea kutoka ofisi moja kwenda ofisi nyingine kusaka taarifa bali kwakupitia mfumo wa iMES kila kitu mtu atafanya akiwa mezani kwake.
“Kwakuwa sisi watumiaji wote tumesha tengenezewa akaunti za kutuwezesha kuingia katika mfumo, hata kama kuna hoja za ukaguzi ambazo zilijitokeza kutoka kwa Mkaguzi Mkuu na Mdhibiti wa Hesabu za Serikali, nikiwa kwenye dawati langu nitaweza kuzifatilia na kuzifanyia kazi bila yakutembea toka Ofisi moja hadi nyingine cha msingi hapa nikwa wataalam kuutumia mafumo kwakuweka data kwa wakati” alisema Limi.
Naye Rose Nyemele, Afisa Muuguzi katika Manispaa hiyo, yeye anasema, pamoja na kutumia mfumo wa (Data Health Information System-DHIS-2) katika masuala ya mipango ya bajeti na MTUHA, ambayo yalianzia ngazi ya Kijiji bado anaona iMES imekuja kwa wakati mujarabu kujibu masuala mtambuka kutoka sekta zote.
“Kwetu sisi watu wa Afya data ni kila kitu, Masuala kama Mipango ya bajeti katika Dawa, Rasilimaliwatu, pamoja na vifaa tiba na vitendanishi vingine hutegemea sana uwepo wa taarifa sahihi na kwawakati, hivyo iMES tunaiona kama suluhu yakudumu, alisema Nyemele.
Mtazamo wa Nyemele, hautofautiani na Afisa TEHAMA katika Halmashauri hiyo Isac Tenguye, ambaye anasema katika Dunia ya sasa kuwa na Mfumo kama huo ni muarobaini wa matatizo ya taarifa.  
“Huu ni mfumo utakao kuwa na chanzo kimoja cha taarifa na utaepusha takwimu kutofautiana kama kipindi cha nyuma, mnaweza kwenda kwenye mkutano mmoja na wadau lakini wewe mtendaji na mdau taarifa zenu mkakuta zinakinzana, lakini kwa iMES tunaona kabisa kila mmoja atajikita kupata taarifa kutoka katika mfumo na hivyo kuondoa tofauti” alisema Tenguye.
Hata hivyo Wataalam hao, hawakusika kuipongeza Serikali pamoja na Wadau wa Maendeleo nchini USAID, chini ya Maradi wa Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma PS.3 kutokana na juhudi wanazo zifanya za uimarishaji wa mifumo ya Sekta za Umma.
“Uzalendo nikuwa na mapenzi mema na nchi yako hivyo tunawapongeza sana OR TAMISEMI pamoja na PS.3, kwa ushirikiano huu ambao unaonesha matunda ya wazi wazi kwa nchi hususan ni katika kipindi hiki cha serikali ya awamu ya tano ambayo imejipambanua katika kumjali mwananchi” alisema Nelson Rugaimukamu Daktari wa Mifugo katika Manispaa hiyp    
Halmashauri ya Jiji la Mwanza, Manispaa ya Ilemela pamoja na Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi mkoani Mwanza, zimekuwa Mamlaka za mwanzo kabisa za majaribio ya mfumo huo wa iMES huku lengo likiwa nikuzifikia Halmashauri zote 185 nchini lakini pia kujumuisha  Wizara  za kisetakta kote nchini.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.