ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, June 1, 2019

RAIS MSTAAFU MWINYI AKABIDHI ZAWADI WASHINDI WA MASHINDANO YA KUHIFADHI KURANI KIKWAJUNI

 Mshindi wa Mashindano ya Kuhifadhi Kurani Juzuu Kumi na Tano, Abdallah Hassan, akibeba zawadi ya televisheni aliyokabidhiwa na Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili, Alhaji Ali Hassan Mwinyi (watatu kushoto), wakati wa fainali za mashindano yaliyofanyika leo  katika Viwanja vya Mapinduzi, Visiwani Zanzibar.Wakwanza ni Mbunge wa Jimbo la Kikwajuni, Mhandisi Hamad Masauni. Picha na Mpigapicha Wetu
 Rais  Mstaafu  wa  Awamu  ya Pili, Alhaji Ali Hassan Mwinyi, akimkabidhi zawadi  Mshindi  wa Mashindano ya Kuhifadhi Kurani Juzuu Tano, Asia Abdallah  wakati  wa fainali za mashindano hayo yaliyofanyika leo, katika Viwanja  vya  Mapinduzi, Visiwani  Zanzibar.Wakwanza  ni  Mbunge wa  Jimbo la Kikwajuni, Mhandisi  Hamad Masauni. Picha na Mpigapicha Wetu
 Mshiriki wa Mashindano ya Kuhifadhi Kurani katika Jimbo la Kikwajuni, Thureiya  Abdallah akisoma  Kurani  wakati  wa  mashindano  hayo  yaliyofanyika leo katika Viwanja vya Mapinduzi Visiwani Zanzibar.Picha na Mpigapicha Wetu
 Mbunge  wa  Jimbo  la  Kikwajuni, Mhandisi  Hamad  Masauni (kulia), akimkabidhi  zawadi  Mgeni Rasmi  katika  Mashindano  ya  Kuhifadhi  Kurani, Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili, Alhaji  Ali Hassan  Mwinyi.Mashindano hayo yamefanyika leo katika Viwanja vya Mapinduzi Visiwani Zanzibar.Picha na Mpigapicha Wetu
Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Mkoa wa  Mjiini, Twalib Ali Twalib  akikabidhi msaada  wa  vitabu  vitakavyoenda katika madrasa mbalimbali Visiwani  Zanzibar  kwa  Mgeni Rasmi  katika  Mashindano  ya  Kuhifadhi Kurani, Rais  Mstaafu  wa  Awamu  ya  Pili, Alhaji  Ali Hassan Mwinyi, wakati wa Mashindano  ya  Kuhifadhi  Kurani  yaliyofanyika  leo Visiwani Zanzibar.Wakwanza kulia ni Mbunge wa Jimbo la Kikwajuni, Mhandisi Hamad Masauni na anayefuatia ni Mwakilishi wa jimbo hilo, Salehe Nassor JazzeraPicha na Mpigapicha Wetu

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.