ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Tuesday, June 4, 2019

RAIS MAGUFULI KUZUNGUMZA NA WAFANYABIASHARA WADOGO 1,000

Dar es Salaam. Miezi mitano baada ya kukutana na wachimbaji wadogo wa madini, Rais John Magufuli anatarajia kuzungumza na takriban wafanyabiashara wadogo 1,000 Ijumaa ya wiki hii.Miezi mitano baada ya kukutana na wachimbaji wadogo wa madini, Rais John Magufuli anatarajia kuzungumza na takriban wafanyabiashara wadogo 1,000 Ijumaa ya wiki hii.
Kwa mujibu wa tangazo lililotolewa na Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), kila halmashauri (zipo 186) inatakiwa kuwaalika wafanyabiashara watano ambao watahudhuria mkutano huo utakaofanyika kuanzia saa 2:00 asubuhi katika ukumbi wa mikutano wa Kikwete, Ikulu jijini hapa.
Agizo hilo lililotolewa Mei 31, liliwataka wakuu wa mikoa yote Tanzania Bara kuwasilisha majina hayo hadi Juni 2. “Orodha hiyo ionyeshe jina, aina ya biashara na namba ya simu ya mfanyabiashara husika, iwapo katika wilaya husika kuna mfanyabiashara ambaye pia ni kiongozi wa kisiasa au mtendaji wa Serikali wasisite kumpendekeza na wafanyabiashara hao wajigharamie,” inasomeka sehemu ya barua hiyo.
Akizungumza Mwananchi kuhusu mkutano huo, Waziri wa Viwanda na Biashara, Joseph Kakunda alisema ajenda kuu ni kusikiliza kero na malalamiko kutoka kwa wafanyabiashara wanaowahudumia wananchi.
Kama alivyokutana na wachimbaji wadogo mapema Januari, Kandege alisema hii ni mara ya kwanza kukutana na kundi hilo, mara zote huzungumza na wenye viwanda vikubwa na wafanyabiashara wa kimataifa.
Alifafanua kuwa kazi ya kuwakusanya wafanyabiashara hao watano kutoka katika kila wilaya itaratibiwa na halmashauri husika chini ya uangalizi wa wakuu wa wilaya.
CHANZO: MWANANCHI

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.