ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Monday, June 3, 2019

SARE NA PAMBA DIMBA LA NYAMAGANA, KAGERA YAJIWEKA PAZURI


TIMU ya Kagera Sugar imejiweka kwenye nafasi nzuri ya kubaki Ligi Kuu ya Tanzania Bara baada ya kulazimisha sare ya 0-0 na wenyeji Pamba SC jioni ya leo Uwanja wa Nyamagana mjini Mwanza.

Mchezo huo wa kwanza wa mchujo wa kuwania kubaki na kupanda Ligi Kuu, ulikuwa mkali na wa kusisimua na Pamba SC watajilaumu wenyewe kwa kushindwa kutumia nafasi walizotengeza.

Kikosi cha Pamba SC kilikuwa; Deus Tilusubya, Hassan Kabailo, Amos Ikuzungura, Alex Joseph, John Mtobesya, Salum Ally, Yussuf Dunia, Salum Juma, Shija Mkina, Elias Seth/Kelvin John dk69 na Ally Rajab/David Richard dk84. 
 Kagera Sugar; Ramadhani Chalamanda, Mwaita Gereza, David Luhende, Juma Nyosso, JUma Shemvuni, Peter Mwalyanzi, Suleiman Mangoma, Ally Ramadhani, Ramadhani Kapera, Paul Ngalyoma/Jerson Tegete dk68 na Venende Ludovic/Japhet Makalai dk53.
John Mongella ndiye aliyekuwa mgeni rasmi wa mchezo huo kati ya Pamba Sc iliyokaribisha Kagera Sugar dimba la Nyamagana jijini hapa akisalimiana na benchi la ufundi pamoja na wachezaji wa akiba wa timu ya Kagera Sugar. 

Hadi mwisho timu hizo zilitoshana nguvu kwa sare ya 0-0.
Sasa Kagera Sugar wanarejea nyumbani Bukoba kujipanga kwa mchezo wa marudiano Jumamosi ya tarehe 8 mwezi huu Juni 2019 katika dimba la  Kaitaba, wakihitaji ushindi ili kusalia Ligi Kuu.
Kagera Sugar wameangukia katika Play-Off baada ya kumaliza nafasi ya 18 kwenye Ligi Kuu ya Tanzania Bara, wakati Pamba SC ilimaliza nafasi ya pili kwenye Kundi B.
Baada ya mchezo huo tumezungumza na wadau wa vikosi vyote tukianzia na benchi la ufundi la klabu ya Wanakawekamo Tupuisant Lindanda al-maarufu Pamba Sports Club kuahirishwa kwa mchezo huu jana kumeathiri chochote?

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.