ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, May 4, 2019

PICHA: WAZIRI MKUCHIKA AWATEMBELEA WAJANE WA HAYATI SOKOINE.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Kapt (Mst) George Mkuchika (Mb), akiongozana na wajane wa aliyekuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Hayati Edward Moringe Sokoine, mama Napono Sokoine na Nakiteto Sokoine na baadhi ya wanafamilia kuelekea kwenye kaburi la Hayati Sokoine alipoitembelea familia hiyo nyumbani kwao Monduli, jijini Arusha ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa majukumu yake.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Kapt (Mst) George Mkuchika (Mb), akisali na wajane wa aliyekuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Hayati Edward Moringe Sokoine, mama Napono Sokoine na Nakiteto Sokoine na baadhi ya wanafamilia kwenye kaburi la Hayati Sokoine alipoitembelea familia hiyo nyumbani kwao Monduli, jijini Arusha ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa majukumu yake
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora,  Kapt (Mst) George Mkuchika (Mb), akimkabidhi kadi ya bima ya afya mjane wa aliyekuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Hayati Edward Moringe Sokoine, mama Nakiteto Sokoine alipowatembelea wajane wa Hayati Sokoine nyumbani kwao Monduli, jijini Arusha ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa majukumu yake

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.