ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, May 3, 2019

UDHANIAYE NDIYE KUMBE ..... MLEVI AMTWANGA MONGELLA SWALI KUNTU



WAHENGA wanamsemo wao 'Umdhaniaye ndiye kumbe siye' hapa wakimaanisha kuwa wengi iwe ndani ama nje ya jamii yetu huwa na tabia ya kuhukumu kwa kutazama muonekano wa nje ya mtu kwamba eti unatafsiri ubora wa mawazo ya mtu, laa hasha, hata walio dhoofu katika suala la muonekano wanaouwezo wa kuibua masuala yaliyo muhimu katika safari ya utatuzi wa changamoto.

Ni katika ziara ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza John Mongella aliyoifanya wilayani Kwimba kukagua maendeleo ya utekelezaji wa miradi mbalimbali, ikiwemo Afya, Elimu, Maji, Barabara, Viwanda, Uchumi na Biashara akiwa katika mkutano kwenye eneo la Hungumalwa anakutana na jamaa huyo aliyekuwa ameutupika nzwii aka kalewa (haikujulikana ni pombe gani) na kumpa kipaza sauti ili kuwasilisha hoja yake........kwani alionekana kupaza sauti kila mara kama mwenye shauku ya kutaka ufafanuzi wa jambo.

Katika ziara hiyo Mongella alikuwa ameandamana na Mbunge wa Jimbo la Kwimba Shanif Mansour, Katibu Tawala wa Mkoa, Wataalamu wa idara mbalimbali pamoja na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya mkoa.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.