ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, May 29, 2019

Four Ways na Girls Queens kuingia kambini rasmi kujiandaa na Castle Africa 5s 2019.




Balozi wa Castle Lager  Africa 5s, Ivo Mapunda (kushoto) akizungumza na wachezaji wa timu ya Four Ways Fc ya Kinondoni na Girls Queens ya Msimbazi Kariakoo zinazo wakilisha nchi kwenye fainali za mashindano ya Castle Africa 5s wakati wa uzinduzi wa Kambi maalumu ya maandalizi  wa mashindano hayo yanayo tarajiwa kufanyika Juni 7 na 8,2019 katika Uwanja Taifa wa Zamani jijini Dar esSalaam.

 Jumla ya Nchi nane(8) zinatarajiwa kushiriki fainali hizo mwenyeji akiwani Tanzania.


Wachezaji wa Four Ways Fc  ya Kinondoni na Girls Queens ya Msimbazi Kariakoo zote za jijini Dar es Salaam wakifanya mazoezi wakijiandaa na fainali za mashindano ya Castle Africa 5s yanayotarajiwa kufanyika Juni 7 na 8,2019 katika Uwanja Taifa wa Zamani jijini Dar esSalaam. Jumla ya Nchi nane(8) zinatarajiwa kushiriki fainali hizo mwenyeji akiwa ni Tanzania.



Four Ways na Girls Queens kuingia kambini rasmi kujiandaa na Castle Africa 5s 2019.
Na Mwandishi Wetu.

TIMU Four Ways Park Fc yenye makazi yake Kinondoni jijini Dar es Salaam na Girls Queens yenye makazi yake Msimbazi Kariakoo jijini Dar es Salaam wameingia kambini leo rasmi kujiandaa na mashindano ya Castle Africa 5s(5 – aside) yanayotarajia kuanza kutimua vumvi Juni 7 na 8,2019 katika Uwanja wa Taifa wa Zamani(Shamba la Bibi) jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na waandishi wa habari Balozi wa Castle Lager Africa nchini Tanzania, Ivo Mapunda alisema timu zote ziko vizuri tayari kwa kuwakilisha Watanzania katika fainali za Kimataifa na ushindi ni lazima kulingana na maandalizi waliyonayo na watakayoendelea nayo.

Mwaka huu Tanzania tutawakilishwa na timu ya Wanaume kutoka Four Ways ya Kinondoni na timu ya Wanawake ya Girls Queens kutoka Msimbazi Kariakoo kwa ujumla timu zote ziko sawa na ziko tayari kwa fainali hizo na leo rasmi sasa wanaingia kambini kwa kujiandaa na fainali hizo.

Nae Meneja wa Bia ya Castle Lager, Pamela Kikuli alizitaji Nchi shiriki zinazotarajiwa kushiriki mashindano hayo ya Africa 5s kuwa ni Africa Kusini, Zambia, Zimbabwe, Swaziland, Lethoto, Uganda, wenyeji Tanzania na chi alikwa ya Nigeria.

Kikuli alisema Nchi hizo zikiwakilishwa na timu ya Wanaume na Wanawake zinatarajiwa kuwasili nchini Juni 5,2019 tayari kwa fainali za Castle Africa 5s.

Juni 6,2019 timu zitakabidhiwa vifaa vya michezo katika Hoteli ya Lamada jijini Dar es Saalaam tayari kwa kuanza mashindano rasmi Juni 7 na 8,2019.

Tunawaomba watanzania wapenda michezo wajitokeze kuja kuzishangilia timu zao zinazowakilisha nchi katika Fainali hizo za Castle Africa 5s.

Mwisho Kikuli alisema fainali hizo zinatarajiwa kuhudhuria na Balozi wa Castle Africa 5s, Samwel Eto’o hivyo tujitokeze kwa wingi kuja kumshuhudia mchezaji mkongwe wa Zamani pamoja na kupiga nae picha.

wameibuka mabingwa katika Bonanza kubwa la Soka  lililofanyika mwishoni mwa wiki katika Viwanja vya Posta Kijitonyama kwa udhamini wa Kampuni ya Bia nchini (TBL) kupitia bia yake ya Castle Lager na hivyo kuzawadiwa Kikombe, Medali za dhahabu, Pesa taslimu shilingi 1,500,000/=, Caton ya bia ya Castle Lager pamoja na kuwakilisha nchi katika fainali za Caslte Africa 5s zinazotarajiwa kufanyika mwaka huu jijini Dar es Salaam ambapo Tanzania itakuwa mwenyeji wa mashindano hayo.

Four Ways Park Fc waliutwaa ubingwa kwa point 7 wakifuatiwa na Jacks Pub Fckwa pont 4 ambao walizawadiwa Medali za Silva, Catoni ya bia ya Castle Lager na pesa taslimu Shilingi 900,000/=

Mshindi wa tatu ni katika fainali hizo ni Meeda Night Club Fc ambao walipata pointi 3 na hivyo kuzawadiwa medali feddha, Caton ya bia ya Castle Lager pamoja na pesa taslimu Shilingi 600,000/=

Akizungumza na wachezaji, waandishi wa habari pamoja na wakazi wa jiji la Dar es Salaam waliojitokeza kwenye Bonanza hilo, Menager Bia ya Castle Lager, Pamela Kikuli alianza kwa kuwapongeza mabingwa Four Ways Park Fc kwa kutwaa ubingwa wa mashindano hayo ikiwa ni mara ya pili sasa kufanyika kwa Tanzania  na akawaomba zawadi walizopata zikawe chachu ya maandalizi bora ya fainali za Castle Afica 5s ambazo zinatarajiwa kufanyika nchini Tanzania.

Kikuli pia aliwapongeza timu ya pili nay a tatu kwa ushindi na akato pongezi kwa timu shiriki zote kwa kujitoa kwao katika fainali hizo na kwa jinsi hiyo wakajiandae kwa mashindano mengine mwakani.

Pamela aliutaja mchakato ulivyokuwa wa kuzipata timu ambao ulianzia kwenye Baa 60 za jijini Dar es Salaam ambapo Bar zilishindana kwa kununua Bia za Castle Lager na kukusanya vizipo na mwisho tukapata timu 32 zilizoongoza na ndizo zimeweza kushiriki Bonanza mpaka kumpata Bingwa ambaye ni Four Ways Park Fc.

Nae Balozi wa Bia ya Castle Africa 5s Tanzania, Ivo Mapundaaliishukuru Kampuni ya Bia Nchini(TBL) kwa uratibu mzuri wa mashindano ya Castle Africa 5s mwaka huu kwani yamekuwa na hamasa ya hali ya juu na kuwaomba waendelee kudhamini mashindano hayo kwani kupitia Bonanza hili wapo waliopata marafiki na mambo mengine mengi kwa sababu ya Bonanza hili kupitia Bia ya Castle Lager ambayo imetuunganisha pamoja.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.