ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, May 9, 2019

DHAHABU ILIYOUZWA SIKU 4 YAIZIDI ILIYOUZWA MWAKA MZIMA - SOKO LA MADINI LABAINI

VIDEO YAJA HIVI PUNDE

Soko la Madini jijini Mwanza tayari limekwisha zinduliwa mkoani Mwanza, naye Waziri wa Madini Dotto Biteko ndiye aliyesimamia hafla fupi iliyofanyika katika jengo maarufu la kibiashara Afrika Mashariki Rock City Mall ambapo amengaza kufutwa kwa kodi zilizokuwa kandamizi kwa wachimbaji wadogo na wafanyabiasha wa madini.

Kwa mujibu wa Biteko, faida za masoko ya madini zimeanza kuonekana kwani katika kipindi kifupi mathalani wilaya ya Chunya ambayo ilikuwa inaongoza kwa utoroshaji wa madini ya dhahabu nchini ndani ya siku 4 tangu soko lianzishwe imeuza Kilogram 22 ambazo hapo awali zilikuwa hazifikiwa hata kwa mauzo mwaka. 

Kwani hapo awali kwa mwaka ilikuwa inauza kilogramu 12 tu ....ambazo zilikuwa zikipita katika mfumo wa uuzaji wa Serikali tizama wizi huo. Audio ndani ya mail.

Faida moja wapo ni kuzuia uuzwaji wa madini kiholela...watu walikuwa wakichimba Tz na kuyakimbizia Kenya na Uganda nako ndiko walikuwa wakiyabrand kwamba yametoka kwao hivyo kuishusha Tz kwenye takwimu za soko la madini la dunia.....

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.