ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, April 5, 2019

"ZIARA YA BUNGENI DODOMA IMENIJENGA" ASEMA PIERRE WAKATI AKIBUSU ARDHI YA MWANZA


MKALI anaye-trend hivi sasa kwa vituko na burudani katika vyombo mbalimbali vya habari ikiwemo mitandao ya kijamii Pierre Gumbo aka 'Konki Liquid' amesema kuwa ziara yake aliyoifanya hivi karibuni Bungeni Jijini Dodoma imemjenga sana.

Pierre ameyasema hayo mapema asubuhi ya leo wakati alipotua jijini Mwanza majira ya saa 1 na dakika 30 kwaajili ya kujoin na wana wa jiji hilo la miamba kula weekend, ingawa ameficha kipi alichong'amua kwamba atakwenda kukifanyia kazi lakini amekiri kuwa ni moja kati ya matembezi yenye faida aliyoweza kuyafanya maishani.

Huku akikwepa maswali ya siasa Pierre amejibu swali alipoulizwa 'Iwapo akikutana na Mhe. Rais Magufuli ni kitu gani atakachomwambia' 

Jeh Pierre Konki ni shabiki wa timu gani, jamaa gani anayemchukia na Jeh kuna vitu asivyovipenda kwenye maeneo ya bata?

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.