ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, April 13, 2019

TUPO TAYARI KUKABILIANA NA TISHIO LOLOTE LITAKALOJITOKEZA - JENERALI MABEYO.



Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi wa Tanzania, Jenerali  Venance Mabeyo amesema kuwa hali ya usalama kwenye nchi ni shwari na wakati wote wapo tayari kukabiliana na matishio yoyote yatakayojitokeza.
Jenerali Mabeyo ameeleza hayo leo wakati wa hafla ya  uzinduzi wa mji wa kiserikali uliojengwa Ihumwe mkoani Dodoman ambao unazinduliwa  na Rais wa Tanzania, John  Magufuli.

“Hali ya usalama kwenye mipaka yetu ni shwari, ndani ya nchi yetu JWTZ kwa kushirikiana na vyombo vya wengine liko tayari kuwalinda wananchi na mali zao, wakati wote tupo tayari kukabiliana na matishio yoyote yanayojitokeza," amesema.

Kuhusu ujenzi wa nyumba na ofisi za Serikali, Jenerali Mabeyo amesema kwa kiasi kikubwa kazi hiyo imefanywa na vijana wa JKT na imefanyika kwa miezi mitano.
Rais Dkt.Magufuli anazindua Mji mpya wa Serikali Uliojengwa Mtumba Jijini Dodoma ambapo unahusisha ofisi za Wizara mbalimbali za Serikali n.k

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.