ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, April 3, 2019

PEMBE ZA NDOVU ZAMPONZA ASKARI MAGEREZA.


Askari Mageraza wa gereza la Msalato A.8070 SSGT Cosmas Ndasi (51) anashikiliwa na jeshi la polisi kwa tuhuma za kukutwa na pembe za ndovu vipande  sita vyenye thamani ya sh 103.5 milioni.

Kamanda wa Polisi mkoa wa Dodoma Gilles Muroto akiongea na waandishi wa habari leo jijini hapa amesema kuwa mtuhumiwa huyo alikamatwa April mosi mwaka huu katika mtaa wa Kilimani  akiwa na vipande hivyo vya pembe vyenye uzito wa kilogramu 13 sawa na tembo watatu.

“Tulitengeza mtego na Askari huyo akanasa na  kumkamata akiwa ameficha kwenye mfuko vipande vya pembe za ndovu kwa ajili ya kumsubiri mteja ili kufanya mauzo,” amesema Muroto.

Katika tukio jingine  Muroto amesema kuwa  wanamshikilia Ambokile Mwampulo (32) kwa tuhuma za kujifanya afisa usalama wa Taifa na kudanganya watu ili kujipatia fedha.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.