ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, April 3, 2019

WAPITISHA SHERIA KALI KUPAMBANA NA USHOGA, WATAKAOTHIBITIKA KUPIGWA MAWE HADI KUFA.



Taifa la Brunei limeazisha sheria, itakayoruhusu wale watakaobainika kushiriki mapenzi ya jinsia moja kuuawa kwa kupigwa mawe. Sheria ambayo imekosolewa na wanaharakati wa haki za binadamu.

Sheria hiyo inaanza kutekelezwa leo Jumatano, lakini pia wale watakaobainika kuhusika na makosa mengine kama wizi, watakatwa mikono.

Uongozi wa taifa hilo dogo la Asia Mashariki limesema limeamua kutekeleza sheria ya Kiislamu (Sharia) hatua ambayo imeshtumiwa na Mashirika ya kimataifa ya kutetea haki za kibinadamu.

Wakati huo huo Ufaransa imeomba Brunei kufuta adhabu ya kifo kwa watu wanaojihusisha na mapenzi ya jinsi moja ikibaini kwamba sheria hiyo inakiuka sheria za kimataifa za haki za binadamu.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.