ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, March 20, 2019

HUDSON KAMOGA AZUNGUMZIA UMUHIMU WA MAAFISA UHUSIANO WA SERIKALI KUPIGWA MSASA


Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu Mkoani Manyara, Hudson Kamoga amefunguka umuhimu wa Maafisa Mawasiliano wa Taasisi mbalimbali nchini kushiriki Kazi Darasa kupitia kikao cha wadau hao kinachoendelea katika ukumbi wa Chuo Cha Benki Kuu ya Tanzania (BOT) Mwanza.

Mada mbalimbali zimewasilishwa ndani ya kikao kazi hicho, zikiwemo mada kuhusu Vichocheo na Mazingira ya Rushwa kwa Maafisa Habari na Namna ya Kukabiliana Navyo, Wajibu wa Maafisa Habari Kuzingatia Usalama wa Nchi Katika Kutekeleza Kazi zao, pamoja na mada ya TUNATEKELEZA2019-Mageuzi Katika Utekelezaji wa Serikali Mikoani na Mbinu zinazotumika Kuuhabarisha Umma.

Mada nyingine zilizo kwenye ratiba ambazo zinategemewa kuwasilishwa ni pamoja na Mjadala wa Kujadili "FAKE NEWS" katika Kazi za Maafisa Habari na jinsi ya kukabiliana nazo na mwisho wadau hao watafungua jukwaa la kuainisha Changamoto za Kada yao na kusaka utatuzi wake.

Kikao Kazi hicho kinatarajiwa kufungwa ijumaa ya wiki hii.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.