ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, March 29, 2019

BAADA YA KIFO CHA MWANANCHI KUANGUKIWA MAWE DC APIGA MARUFUKU SHUGHULI ZA UCHIMBAJI



HALI ya mazingira hatarishi kwa shughuli za uchimbaji mchanga kwenye eneo la vilima vya Mahina tambukareli wilayani Nyamagana mkoani Mwanza imemlazimu Mkuu wa wilaya ya Nyamagana Philis Nyimbi kupiga marufuku wananchi au mtu yeyote kufanya shughuli za uchimbaji kwenye eneo hilo.

Mwili wa Ndalahwa Mashauri aliyeangukiwa na mawe akiwa shimoni kwenye machimbo ya udongo wa mfinyanzi al maarufu MABUMBA tangu Jumatatu ya tarehe 24 mwezi Machi 2019 hatimaye  Alhamisi ya tarehe 28 Machi 2019 umefanikiwa kutolewa  shimoni humo.

Kwa muda wa siku nne waokoaji wamekuwa katika eneo la ajali kwenye vilima vya kata ya Mahina, Tambika reli wakijaribu kwa kila namna kuona ni jinsi gani wanafanikiwa kuutoa mwili wa marehemu Mashauri ambaye alikuwa ameangukiwa na mawe pamoja na kisusi cha udongo mita kadhaa ardhini wakati akichimba udongo.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.