ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, March 30, 2019

MSANII WA MAREKANI NIPSEY HUSSLE AUAWA KWA KUPIGWA RISASI.


Rapa wa Marekani,  Ermias Davidson maarufu kama Nipsey Hussle ameuawa kwa kupigwa risasi mapema leo nje ya duka lake la nguo lililoko Los Angeles.

Nipsey mwenye umri wa miaka 33, alipigwa risasi kadhaa mwilini mwake na alipofikishwa hospitalini alibainika tayari alikuwa ameshafariki, kwa mujibu wa CNN.

Watu kadhaa walijeruhiwa pia katika tukio hilo ambalo kwa mujibu wa polisi lilihusisha makundi mawili kushambuliana kwa risasi, Kusini mwa Los Angeles.

Nipsey alikuwa mmoja kati ya wakali wa rap waliotikisa ulimwengu mpya wa michano, ambapo albam yake ya ‘Victory Lap’ ilifanikiwa kutajwa kwenye kipengele cha albam bora ya rap/hiphop kwenye tuzo za Grammy mwaka huu, kipengele ambacho rapa wa kike Cardi B alifanikiwa kushinda na albam yake ‘Invasion of Privacy

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.