ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Monday, February 25, 2019

MAHAKAMA YASOGEZA MBELE KESI YA MAUAJI YA WATOTO NJOMBE


Mahakama ya hakimu mkazi mkoa wa Njombe leo imewapandisha kizimbani kwa mara ya pili  watuhumiwa watatu wa mauaji ya watoto watatu wa familia moja wa kijiji cha Ikando kata ya kichiwa wilayani Njombe.

Watuhumiwa hao ni Pamoja na JOEL JOSEPH NZIKU,NASSON ALFREDO KADUMA  na ALPHONCE EDWARD DANDA Ambao Wanakabiliwa na Mashtaka ya Kuwaua Watoto Hao Kijijini Humo.

Watoto hao ni pamoja na Godliver Nziku, Gasper Nziku na  Giriad Nziku ambao ni watoto wa familia moja huku ikielezwa kuwa watuhumiwa hao walitenda kosa la kuwaua januari 20 mwaka huu

Hakimu mkazi mkoa wa Njombe Magdalena Ntandu Ameahirisha kesi hiyo hadi tarehe 11 mwezi machi mwaka huu mpaka itakapotajwa tena huku watuhumiwa wakirejeshwa rumande.

kesi hiyo kwa mara ya kwanza ilitajwa mnamo tarehe 12 mwezi wa pili 2019 mbele ya mahakama na wakili mwandamizi wa serikali Ahmed Seif.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.