ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, November 15, 2018

WAFANYABIASHARA ENDELEENI KULIPA KODI:- DKT ABBASSI

Mkurugenzi   wa   Idara   ya   habari  Maelezo   na   msemaji  Mkuu wa Serikali, Dkt. Hassan Abbassi 

Na Grace Semfuko-MAELEZO

Wafanyabiashara   nchini   wametakiwa   kuendelea   kulipa   kodi   na   kuzingatia   matumizi   yamashine za kielektroniki za kukusanyia mapato (EFD) ili wasiingie katika migogoro isiyo yalazima na serikali. 

Hayo   yamesemwa   jana na  Mkurugenzi   wa   Idara   ya   habari  Maelezo   na   msemaji  Mkuu wa Serikali, Dkt. Hassan Abbassi katika mahojiano maalum na redio Uhuru ya Jijini Dar es Salaa,kuelezea mafanikio ya Serikali ya Awamu ya Tano katika kipindi cha miaka mitatu tangu iingiemadarakani.

“Wafanyabiashara wale wanaokwepa kulipa kodi, tutawafikia, ni mkuhimu ulipe kodi ili iwezekufanya kazi za kuwahudumia watanzania, na kwa  mawakala wa kukusanya kodi wahakikishewanaifikisha kodi hizo serikalini kwa wakati” alisema. 

Dkt Abbasi amesema Serikali ya Awamu ya Tano ya Rais Magufuli  inafanya kazi kubwa  yakuhakikisha Watanzania wanapata maisha bora, hivyo ulipaji wa kodi ni muhimu sana ili fedhahizo ziwezeshe kupatikana kwa huduma bora zaidi kwa watanzania. 

Aidha  Dkt. Abbassi amewataka watendaji kwenye taasisi za umma kufanya kazi kwa weledina  kwa  kujituma   pia   kuzingatia   majukumu   yao   yaliyopo   kwenye   mikataba  yao   ya   kazi   ilikuleta ufanisi  kwenye taasisi zao. Alisema  Serikali haitasita kuwachukulia hatua za kinidhamu watendaji wote wa umma ambaohawawajibiki ipasavyo  kwani  wamekuwa  ni  mzigo kwa Serikali, na wanakwamisha  jitihadakubwa zinazofanywa na Rais Magufuli.

“Mmeona   wenyewe   juzi   tu   Mheshimiwa   Rais   amefanya   maamuzi   magumu   lakini   ni   sahihikabisa ya kuwaondoa baadhi ya watendaji wasiowajibika Serikalini,haiishii kwenye ngazi yajuu tu hii ni kwa kila mtendaji wa Serikali kuanzia ngazi za chini” alisema Dkt. Abbassi. 

Dkt.Abbasi   alisema  kuna   mjadala   mkubwa   duniani   unaendelea   kuhusu   maendeleo   na   ninimaana ya kuwekeza, ambapo Tanzania imewekeza kwenye miradi mbalimbali ya maendeleona  miundombinu pamoja na watu kwa maana ya watumiaji wakuu wa miradi hiyo.

Kuhusu elimu amesema serikali inatoa shilingi bilioni 23.85 kila mwezi ili kugharamia elimukwenye shule za Serikali ikiwa ni mojawapo ya mkakati wa kuimarisha elimu nchini na hasakatika utekelezaji wa sera ya Serikali ya elimu bure kuanzia ngazi ya awali mpaka kidato channe.

Fedha hizo zinapelekwa moja kwa moja kwenya akaunti za shule badala ya kupelekwa kwenyeHalmashauri za Wilaya na Manispaa ambazo zilikuwa zikichelewesha fedha hizo kufika shuleniama kutumiwa kwa matumizi yaliyokusudiwa.

Serikali pia imeongeza  fedha za mikopo ya  wanafunzi wa elimu ya juu   katika  kipindi chamiaka mitatu  ya  utawala   wa  Rais  Magufuli kutoka  shilingi  Bilioni  380  mwaka 2015  mpakakufikia zaidi ya bilioni 500 mwaka 2018.Hatua hiyo ya Serikali inalenga kuimarisha sekta ya elimu nchini ambayo inatajwa kuwa nimsingi mkuu wa maendeleo endelevu kwenye Taifa lolote Duniani.MWISHO

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.